Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali ambayo ni mazuri na nashukuru pia kwamba mradi unaenda vizuri kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri. Sasa maswali mawili:-

Swali la kwanza ni nini kauli ya Serikali kuhusu bei ya maji maana hata kule ambako miradi imekamilika kuna mahali ambako bei ya maji ni kubwa sana hadi shilingi 5,000 kwa unit ambazo ni lita 1000, kama kule Kyamurairi na sehemu nyingine ambako maeneo mengine ni shilingi 1000 lakini kule ni shilingi 5,000.

Swali la pili, kuna Kata Sita ambazo nako kuna mradi unaosemwa siku nyingi Kata ya Izimbya, Kaitoke, Mugajwale, Ruhunga, Katoro na Kaibanja, ambako Mheshimiwa Naibu Waziri amewahi kufika tukazungumzia jambo hilo na anazifahamu Kata hizo, mradi huo unaanza lini kutekelezwa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jasson Rweikiza kama ifuatavyo:-

Awali ya yote ni kweli nilifika na Mheshimiwa Mbunge nakupongeza, tulifanya hii kazi kwa pamoja na tutakuja tena kuona kwamba tunakamilisha miradi hii.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na bei za maji ninaomba kutoa taarifa ni wiki ya jana tu Mheshimiwa Waziri ametoa bei elekezi kwa miradi yote nchi nzima. Hivyo maeneo ambayo yana bei ambazo kidogo siyo rafiki kwa wananchi kama maeneo yako ya Bukoba Vijijini, hata pale Karatu yote tumeyazingatia na bei elekezi zimetolewa na Mheshimiwa Waziri kwa kuzingatia nguvu inayotumika kusukuma mitambo yetu. Kama ni mafuta, kama ni umeme wa jua kama ni mserereko, kama ni umeme wa TANESCO pamoja na pump za mikono, yote haya Mheshimiwa Waziri ameshatoa maelekezo na sasa hivi bei zitakwenda kuwa rafiki sana, wiki ijayo kwa maana ya mwaka mpya wa fedha zitaanza kutumika.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusiana na Kata Sita alizozitaja Mheshimiwa Mbunge tumeshirikiana kwa pamoja na tayari usanifu nafahamu unaendelea, kadri tutakavyopata fedha tutaleta Mkandarasi mapema sana ili Kata hizi zote ziweze kupata maji na maeneo haya ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakipata matatizo ya maji tunakuja kuyashughulikia.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Supplementary Question 2

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkoa wa Dar es Salaam miundombinu yake ya maji ni ya muda mrefu sana, kwa sababu tulipata maji muda mrefu kabla ya Mikoa yote. Sasa hivi miundombinu ile ni mibovu na inamwaga maji mengi hasa katika Jimbo letu la Temeke.

Je, Serikali mna mkakati gani wa kuelekeza tena upya miundombinu ya maji katika Mkoa wetu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dorothy Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna baadhi ya maeneo ya Temeke yana changamoto ya mabomba kupasuka kwa uchakavu na maji sasa yamekuwa mengi kwa sababu ni miradi mikubwa iliyotekelezwa na DAWASA, hivyo nipende kukutoa hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeanza utekelezaji nimeshafuatilia hili maeneo ya Tandika, Tandale maeneo ya Wailess na Temeke penyewe tayari wameanza kubadilisha yale mabomba yaliyochakaa.

Mheshimiwa Spika, maeneo ambayo bado maji yanaendelea kuvuja tunaendelea kufanyia kazi na kadri tutakavyopata fedha tunakuja kukamilisha maeneo yote ambayo maji yanavuja. Hili siyo tu kwa Temeke Waheshimiwa Wabunge niseme Mikoa yote, Majimbo yote tumetoa maelekezo kuhakikisha maeneo ambayo maji sasa yamekuwa ni mengi na mabomba yamechakaa yanashindwa kuhimili presha ya maji haya, tunakuja kufanyia ukarabati.(Makofi)

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Supplementary Question 3

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Tatizo lililopo Bukoba Vijijini linafanana kabisa na tatizo lililopo Mtwara Vijijini. Kata ya Mango Pacha Nne, kuna mradi wa maji hadi leo haujakamilika. Je, ni lini Serikali itamalizia mradi huu ili kumtua ndoo kichwani mama wa Mango Pacha Nne ambaye kwa muda mrefu wamekuwa na changamoto kubwa ya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge amefuatilia hili sana na nimhakikishie nitafika Mtwara vijijini lakini tayari naendelea kusisitiza maelekezo tuliyoyatoa kwa watendaji wetu waweze kufanya kazi usiku na mchana ili mradi ule uweze kukamilika na akinamama na familia zote za Mtwara Vijijini ziweze kunufaika na kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan. Tunampongeza Mama Samia tumeshapata fedha asilimia 95 ya bajeti ambayo tunakwenda kuimaliza hivi punde. (Makofi)

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru mradi wa maji wa Isunga Kadashi ni moja ya miradi ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri aliitembelea katika Jimbo la Sumve na tukaahidiwa kwamba mradi ule utaanza kutoa maji ndani ya miezi miwili, lakini hadi sasa ninapozungumza ni zaidi ya mwaka sasa umepita na mradi ule hautoi maji.

Je nini tamko la Serikali kuhusu kitendo hicho ambacho kinapelekea watu wa Kijiji cha Isunga kutokupata maji kwa muda? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tamko la Serikali kwenye mradi ambao mimi na Mheshimiwa Mbunge tuliutembelea ni kufuatilia na kuhakikisha maji yanatoka, Mheshimiwa Mbunge naomba niwe nimelipokea nilifanyie kazi kwa nini maji hayajatoka hadi sasa. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Supplementary Question 5

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kijiji cha Mrelu ni eneo kame sana na kimeshachimbwa kisima. Je, ni lini Wizara italeta fedha ili maji yale yaweze kusambazwa?

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maji.

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba arudie swali.

SPIKA: Mheshimiwa Hhayuma hujasikika vizuri.

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kijiji cha Mrelu ni eneo kame sana na sasa hivi kisima kimeshachimbwa na wananchi wanaishukuru sana Serikali. Je, ni lini fedha zitapelekwa ili maji yale yaweze kusambazwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hhayuma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mara tunapopata chanzo cha uhakika, kusambaza ni moja ya wajibu wetu mkubwa na hiyo ndio tija ya dhima ya Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Mbunge mwaka ujao wa fedha mapema kabisa miezi ya mwanzoni tunaenda kusambaza maji katika eneo hili ambalo tumechimba kisima.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji Kemondo - Maruku katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika.

Supplementary Question 6

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mradi wa Nduku – Ntobo - Busangi ni mradi uliopangwa kiasi cha shilingi 750,000,000 ili uweze kukamilika na tayari hatua za manunuzi, mabomba yote ya plastiki yamenunuliwa, lakini kimekwamisha tu bomba za chuma.

Sasa je, ni lini Serikali itaenda kulipa fedha ili mabomba haya yaweze kununuliwa na mradi uweze kukamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama yeye alivyokiri ni mradi ambao unakwenda kuleta tija katika eneo hili na tayari baadhi ya mabomba yamefika, bomba hizi za chuma tayari zimeshaagizwa. Tumshukuru Mheshimiwa Rais ametoa fedha nyingi, kazi zimekuwa nyingi, hivyo hata wanaozalisha haya mabomba wamezidiwa, kwa hiyo kidogo kumekuwa na ucheleweshwaji. Hata hivyo, tumeshawaongezea nguvu ya kuona kwamba wanaweza kufanikiwa kuleta mabomba haya ndani ya muda. Hivyo, tunaomba Mheshimiwa Mbunge avute Subira, mabomba ya chuma yanakuna na kazi hii lazima ikamilike.