Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 53 Water and Irrigation Wizara ya Maji 473 2022-06-28

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ushetu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Ushetu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imekamilisha ujenzi wa Miradi ya Maji katika Vijiji vya Kisuke, Igunda na Nyankende. Vilevile utekelezaji wa Miradi ya Maji katika Vijiji vya Mpunze, Sabasabini, Iponyanholo, Itumbili, Mitonga na Ididi inaendelea na inatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2022. Kukamilika kwa miradi hii kutaboresha huduma ya upatikanaji wa maji toka asilimia 58 hadi asilimia 62. Aidha, mpango wa muda mrefu ni kutekeleza mradi utakaotumia chanzo cha maji cha Ziwa Victoria ambapo usanifu utafanyika katika mwaka wa fedha 2022/2023.