Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri wa maji pamoja na timu yake yote kwa kazi nzuri wanayoifanywa kwa miradi ya maji, lakini nina maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Mkoa wa Shinyanga una Majimbo sita na Jimbo la Ushetu ni mojawapo lakini Majimbo matano yana miradi mikubwa ya maji ya Ziwa Victoria isipokuwa Jimbo la Ushetu ambalo ni kilometa kama 17 tu ilipo miradi mikubwa wa maji. Leo hii maji hayo yameenda Tabora, yameenda Shelui, Mkoani Singida. Sasa nataka nipate commitment ya Serikali ni lini sasa maji haya ya Ziwa Victoria yataanza kupelekwa kwa wananchi wa Jimbo la Ushetu?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuongozana na mimi kwenda kushuhudia adha wanayoipata wananchi wa Jimbo la Ushetu hasa katika Kata za Uyogo, Mapamba, Ushetu, Ulowa, Ubagwe na Ulewe ambako sasa wanauziwa ndoo ya maji kwa shilingi 1,500 hadi 2,000? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Cherehani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napokea shukrani za Mheshimiwa Cherehani. Naamini anafahamu wiki iliyopita tayari watendaji wetu kutoka Makao Makuu ya RUWASA walikuwa jimboni kwake na chanzo cha wale watendaji kufika pale ni kwa sababu tunaenda kuanza mradi huu ambao tutachukua maji ya Ziwa Victoria kuleta kwenye maeneo haya ambako miradi inahitajika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kuongozana na Mheshimiwa Mbunge nilishamjibu kwamba baada ya watendaji wetu wataalam wakishamaliza eneo lao, nitakwenda kuongeza hamasa ya kuona miradi hii inatekelezwa ndani ya muda uliopangwa. (Makofi)

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 2

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tarehe 29 mwaka 2021 niliuliza swali la msingi juu ya mradi ya Ziwa Victoria wa kwenda Kata za Goweko, Igalula na Nsololo na majibu ya Serikali hadi kufikia Juni, 2022, utakuwa umekamilika, lakini mradi huu upo asilimia 30. Nataka kauli ya Serikali, je, mradi huu utakamilika lini na wananchi wa Kata za Kigwa, Goweko na Nsololo wataweza kupata maji ya Ziwa Victoria?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Protas, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amekuwa akifuatilia sana huu mradi, lakini changamoto za kiufundi ndizo zilizopelekea mradi huu kusuasua na sasa hivi ufumbuzi umeshapatikana. Mheshimiwa Mbunge kama tulivyoongea avute subira tunakwenda kukamilisha mradi huu na lengo ni kuona wananchi wanapata maji safi, salama na ya kutosha tena bombani.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 3

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahante sana kwa kunipa nafasi. Chanzo cha maji cha Lojo kilichopo katika Kijiji cha Matongo pale Ikungi ni chanzo kikubwa ambacho kilifanyiwa utafiti mwaka 2010.

Je, ni lini sasa Serikali itaweza kukiendeleza chanzo kile ili kiweze kutosheleza maji katika Mkoa mzima wa Singida? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Miraji Mtaturu, Mbunge wa Ikungi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli chanzo hiki tunakitarajia kuwa ni moja ya vyanzo vitakavyopunguza tatizo maji katika eneo lake. Kukiendeleza chanzo hiki mwaka ujao wa fedha tutarudi kuona namna bora ya kutumia maji haya. Lengo ni kuona kwamba tunapunguza tatizo la maji katika eneo lake lote. (Makofi)

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Muleba na hili swali nimeuliza mara nyingi sana hapa Bungeni. Tunapakana na Ziwa Victoria na Wilaya ya Muleba ina matatizo makubwa sana ya maji pamoja na kwamba tupo kando kando ya Ziwa Victoria. Tuna mradi ambao usanifu na upembuzi yakinifu umekamilika wa kuchota maji kutoka ziwa Victoria na kuyasambaza kwenye Kata sita za Gwanseli, Magata, Kabuganga, Muleba Mjini, Buleza, Kagoma na Kikuku. Je, ni lini utekelezaji wa huo mradi utaanza kwa ajili ya wananchi wa Wilaya ya Muleba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ishengoma Kikoyo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru kwa kukiri kwamba pamoja na changamoto hizo lakini kazi zinaendelea kufanyika ndani ya Jimbo lake na hizo kata zote alizozitaja tunaendelea kuzifanyia kazi. Mimi na Mheshimiwa Mbunge tulitembelea chanzo kile kingine pale Kizuri ambacho kinatoa maji mengi na tunakiboresha. Kutumia maji ya Ziwa Victoria tutayatupia kwenye maeneo haya yote ambayo yapo mbali na vyanzo vingine. Maeneo yale ambayo Mheshimiwa Mbunge tumeshaongea mara nyingi na nimefika pale, ambayo yanapata maji tutaendelea kutumia vyanzo vilivyopo. Kwa maeneo ambayo ni muhimu kutumia maji ya Ziwa Victoria, tunakwenda kufanya kazi nzuri na maeneo haya yote aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge tutahakikisha maji yanapatikana.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Mradi wa Maji wa Patandi unaotekelezwa katika Kata ya Keri umeacha vitongoji vinne katika Kata ya Gwarusambo ambako ndiko vyanzo vya maji vinapatikana.

Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuambatana nami kwenda site kutatua hizo changamoto? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nimeshafika Jimboni kwa Mheshimiwa Dkt. Pallangyo na tumefanya kazi nzuri, maeneo ambayo hayakupata maji kwa miaka mingi sasa hivi yanapata. Hivi vitongoji vinne vilivyobaki navyo vinaenda kwenye mwaka ujao wa fedha na vitapata maji. Suala la mimi kufika Jimboni kwa Mbunge, asijali kama ambavyo nilikwenda nikimaliza maeneo ambayo sijafika, nitarudi tena.