Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2023-11-08

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Hospitali ya Wilaya ya Manyoni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetoa shilingi millioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa wodi mbili za wanawake na wanaume pamoja na jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni. Aidha, majengo haya yamekamilika na yataanza kutoa huduma mwishoni mwa Novemba, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepeleka shilingi billioni 1.4 Oktoba, 2023 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri inaendelea na taratibu za kupata mzabuni kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wodi ya wazazi lenye chumba cha upasuaji wa dharura, jengo la X-ray, stoo ya kuhifadhia dawa, jengo la kliniki ya Mama na Mtoto, jengo la kufulia, njia za kutembelea wagonjwa pamoja na kufanya ukarabati wa majengo mengine ya Hospitali ya Wilaya ya Manyoni, ahsante.