Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 54 2024-02-02

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-

Je, lini Mradi wa Maji wa Igongwi utakamilika katika Tarafa ya Igominyi Wilayani Njombe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji nijibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na Utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Igongwi katika Halmashauri ya Mji wa Njombe unaolenga kutatua tatizo la maji kwa wakazi 9,717 waishio katika Vijiji vya Kitulila, Madobole, Luponde na Njoomlole. Hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa asilimia 78.

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mradi huo imekamilisha ujenzi wa vyanzo vinne vya maji, uchimbaji wa mtaro na ulazaji wa bomba kuu kilometa 49.7, ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji umbali wa kilometa 26 kati ya 35, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 32 kati ya 55, ujenzi wa matenki mawili yenye jumla ya ujazo wa lita 100,000 kati ya matenki manne pamoja na ujenzi wa miundombinu sita ya mfano ya kuvuna maji ya mvua iliyojengwa katika Shule za Msingi Madobole na Kitulila, Ofisi ya Serikali ya Kijiji Madobole na Zahanati ya Kijiji cha Kitulila. Kazi zote zilizosalia zinatarajiwa kukamilika kabla au ifikapo mwezi Juni, 2024.