Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, lini Mradi wa Maji wa Igongwi utakamilika katika Tarafa ya Igominyi Wilayani Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Sisi watu wa Mkoa wa Njombe tunatambua kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika Mradi huu wa Maji wa Igongwi. Lakini vilevile tunatambua sababu mojawapo ya kusababisha mradi huu wa Igongwi kutokuendelea ni kutokana na kutopeleka fedha kwenye Mradi wa Maji wa Ruvuyo Wilaya ya Ludewa ambako ndiyo chanzo cha maji kinatokea. Je, lini Serikali itapeleka pesa kwenye Mradi wa Ruvuyo ili kuweza kuruhusu mradi huo wa Igongwi uendelee?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pil; Kuna baadhi ya Vijiji ambavyo viko ndani ya Jimbo la Njombe Mjini kikiwepo Kijiji cha Ihanga havikuwekwa kwenye mradi wa maji vijijini kimakosa. Je, lini Serikali itaweka vijiji hivi ambavyo viko kwenye Jimbo la Njombe Mjini havikuhesabika kama viko vijijini kuwekwa kwenye Mradi wa Maji Vijijini? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Mgaya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze kwa ufuatiliaji. Mheshimiwa Neema hili umeishawahi kuniuliza mara kadhaa na nimeishalifanyia kazi kulingana na ufuatiliaji wako. Ili huu mradi upate kuendelea ni kweli fedha hapa katikati zilisimama lakini tumshukuru sana Mheshimiwa Rais tayari fedha Januari hii tumeanza kupokea ndani ya Wizara. Kwa hiyo, ni moja ya maeneo ambayo tutakwenda kupeleka fedha kwa awamu ili kazi ziweze kuendelea.

Mheshimiwa Spika, Eneo la Njombe mjini hivi vijiji ambavyo havikuhesabika katika miradi ya vijijini, ilifanyika hivyo kwa sababu ya jiografia yake. Lakini kwa ushirikiano wako wewe pamoja na Mbunge wa Jimbo wote mmeweza kufikisha suala na Viongozi wa Mkoa wa Njombe wameishapewa maelekezo kuona kwamba vijiji hivi navyo vinapelekewa huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, lini Mradi wa Maji wa Igongwi utakamilika katika Tarafa ya Igominyi Wilayani Njombe?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mradi wa Maji Awamu ya Pili wa Jimbo la Bukoba Mjini unaohudumia Kata tano; Kata ya Buhembe, Nyanga, Kashai, Kahororo na Nshambya umekwama tokea mwaka jana japokuwa mkandarasi yuko site.

Je, Serikali ipo tayari kupeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 253 kwa dharula ili wananchi wa kata hizi tano waweze kupata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Lugangira, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi unaendelea kutekelezwa ndiyo maana umeweza kusema yule Mkandarasi yuko pale lakini suala la kupeleka fedha milioni 253 ni jukumu la Wizara nikuhakikishie Mheshimiwa Neema hizi fedha zitapelekwa ili kazi ziweze kuendelea. (Makofi)