Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 10 2024-01-30

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, lini mradi wa maji wa vijiji 57 ambao utaanzia Kyerwa, Nyakatuntu mpaka Kimuli Wilayani Kyerwa utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante; kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Seba Bilakwate (Mb) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa maji katika vijiji 57 Wilayani Kyerwa. Hadi sasa, utekelezaji wa mradi huo unaendelea katika vijiji 27 ambavyo ni Nkwenda, Rwabwere, Karongo, Nyamiaga, Nyakatera, Kagu, Masheshe, Nyamweza, Kaikoti, Iteera, Muleba, Chanya, Kimuli, Rwanyango, Chakalisa, Kikukuru, Karambi, Rwele, Mukunyu, Rukuraijo, Makazi, Kibimba na Mabira.

Mheshimiwa Spika, kazi zilizotekelezwa katika miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa matenki matano (5) yenye jumla ya ujazo wa lita 1,450,000, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 110, ujenzi wa vituo 102 na vioski 18. Utekelezaji wa miradi hiyo umefikia wastani wa asilimia 80 na unatarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2024. Mradi utakapokamilikautawanufaisha wananchi wapatao 83,000. Miradi hiyo katika vijiji 30 vilivyobaki itatekelezwa katika mwaka wa fedha 2024/2025.