Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge 128 2024-02-08

Name

Mwantatu Mbarak Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: -

Je, vijana wenye ulemavu wamenufaika vipi na mafunzo na mikopo inayotolewa na Serikali?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantatu Mbarak Khamis, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kutambua umuhimu wa mafunzo na mikopo kwa Vijana wenye Ulemavu inatekeleza mikakati na programu jumuishi mbalimbali inayolenga kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu, mafunzo na ujuzi kwa lengo la kuboresha hali zao za maisha na kukuza ushiriki wao katika shughuli za kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kitabu cha Hali ya Uchumi cha Mwaka 2022, kiasi cha mikopo ya shilingi bilioni 81.3 zilitolewa kwa watu 640,723 wenye ulemavu wakiwemo vijana wenye ulemavu. Mikopo hiyo imewezesha vijana wenye ulemavu kuanzisha au kuendeleza biashara zao na hivyo kupunguza utegemezi na kuwa na uwezo wa kuchangia kwa kiwango kikubwa katika mahitaji yao wenyewe na familia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2022/2023, zaidi ya vijana wapatao 2000 wamenufaika na mafunzo yanayotolewa hapa nchini. Vijana hao wamepata mafunzo ya ufundi stadi na ujasiriamali kupitia vyuo vya ufundi na marekebisho, vyuo vya VETA na kupitia programu ya ukuzaji ujuzi iliyopo nchini, ahsante.