Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantatu Mbarak Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, vijana wenye ulemavu wamenufaika vipi na mafunzo na mikopo inayotolewa na Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa, naipongeza Serikali kwa majibu mazuri. Pia naipongeza Serikali kwa kutambua umuhimu wa kujumuisha vijana wenye ulemavu katika programu mbalimbali. Vilevile, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, napenda kumuuliza swali dogo tu la nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kufuatilia na kuwaendeleza vijana hao ili lile lengo la Serikali liweze kutimia? (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokea pongezi za Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Mheshimiwa Mwantatu lakini na mimi nimpongeze sana Mheshimiwa Mwantatu kwa kazi nzuri anayofanya tangu nimemfahamu katika eneo letu hili la watu wenye ulemavu, anafanya kazi nzuri, lakini nimwambie kwamba, Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia tunaendelea kuweka mikakati ya kuwafikia vijana hawa. Moja, Mheshimiwa Naibu Waziri anayehusika na eneo hili amekuwa akifanya programu za kuwatembelea na kuwaona vijana hawa na hata Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Mheshimiwa Profesa Ndalichako, anapita katika maeneo mbalimbali kuwatembelea kuona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu, kupitia kitengo cha watu wenye ulemavu imeendelea kufanya programu za kuwapitia na kuendelea kuwahamasisha vijana hawa kwa kushirikiana na wenzetu upande wa TAMISEMI, Maafisa Maendeleo ya Jamii, kuona namna wanaendelea vizuri. Lakini mwisho tunafanya mapitia ya Sera ya Taifa ya Watu Wenye Ulemavu ili kuweka mikakati ambayo ni endelevu itakayowezesha kundi hili kuendelea kushiriki lakini niwape moyo na kuendelea kuwaambia wenzangu, watu wenye ulemavu hasa vijana, waendelee kuchangamkia fursa ambazo zinatolewa na Serikali na sisi tuko pamoja na wao. Ahsante.

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, vijana wenye ulemavu wamenufaika vipi na mafunzo na mikopo inayotolewa na Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, imekuwa takribani miezi kumi tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, atoe maelekezo ya kusitisha mikopo iliyokuwa inatolewa kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwa kupisha utaratibu mpya ambao utakuwa na manufaa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua ni lini hasa Serikali itarejesha utaratibu huu, ili vijana waendelee kunufaika na mikopo hii?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Vijana, Mheshimiwa Ng’wasi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili kwa kuwa lilifuata utaratbu na wenzetu wa TAMISEMI, wameendelea kulizungumzia, tuendelee kuwaachia wenzetu wa upande wa TAMISEMI watatupa taarifa rasmi ya wapi wamefikia na lini wataanza kutoa mikopo hiyo, lakini niwahakikishie kwamba, mikopo ile ipo, fedha ipo. Utaratibu utakapoanza makundi haya yajiandae kwa ajili ya kunufaika na programu hiyo.