Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 129 2024-02-08

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka walimu katika shule za sekondari na msingi Wilayani Nyang’hwale?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Tabitha Chagula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2023 Serikali iliajiri Walimu 13,130 ambapo Walimu 20 wa shule za msingi na 55 wa shule za Sekondari walipelekwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale. Serikali inatambua mahitaji ya Walimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale na maeneo mengine. Hata hivyo, kila mwaka Serikali inaendelea kupunguza mahitaji ya walimu katika sekta ya elimu na hivi karibuni Serikali itatangaza ajira za walimu baada ya taratibu za kibali kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi kukamilika na kadri ya upatikanaji wa fedha.