Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 130 2024-02-08

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani kuhusu maboma ya majengo ya Nyumba za Walimu na Madarasa yaliyotelekezwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya tathmini ya maboma ya nyumba za walimu ambapo jumla ya maboma 2,527 yamebainishwa. Ili kukamilisha maboma haya, zinahitajika shilingi bilioni 37.905 na kila boma litagharimu shilingi milioni 15.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa madarasa, jumla ya maboma ya madarasa 10,106 yanayohitaji shilingi bilioni 126.6 yametambuliwa. Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma ya nyumba za walimu na madarasa yaliyoanzishwa na wananchi.