Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu maboma ya majengo ya Nyumba za Walimu na Madarasa yaliyotelekezwa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa majibu. Swali langu la kwanza; kwa nini, Serikali isitoe fedha kwa haraka kukamilisha hayo mabima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, bado kuna upungufu mwingi wa madarasa, je, Serikali inachukua mkakati gani wa kudumu kuhakikisha hali hii haijitokezi tena? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara. La kwanza, kwa nini Serikali isitoe fedha hizi kwa haraka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe ya kwamba, katika Sera ya Ugatuaji wa Madaraka (D-by-D) jukumu la kujenga miundombinu yoyote ya maendeleo katika halmashauri zetu nchini ni jukumu la Halmashauri yenyewe. Serikali Kuu inafanya usimamizi na ku-complement jitihada za wao wenyewe katika zile halmashauri kule. Hivyo basi, ni jukumu la Mkurugenzi kuweza kufanya tathmnini katika eneo lake na kutenga fedha katika fedha za maendeleo kuweza kumalizia nguvu za wananchi zilipokwenda kama kwenye zahanati, vituo vya afya na madarasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha inayotafutwa Serikali Kuu ni kwenda kuongeza tu nguvu na kasi katika eneo husika. Hivyo, basi, Serikali Kuu inaendelea kutafuta fedha hizo kama ilivyotafuta fedha za kuweza kumalizia maboma na kuongeza madarasa katika miaka mingine kama ambavyo kila Mbunge humu ndani na halmashauri yake walipata shule mpya kupitia Mradi wa SEQUIP na Mradi wa BOOST.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikkienda kwenye swali lake la pili; hali hii itaendelea kuwa hivi kwa sababu, elimu ya awali ni bure, kwa Sera ya Serikali yetu hii. Elimu ya msingi ni bure, elimu ya sekondari ni bure kwa hiyo, idadi huongezeka kadiri mwaka unavyokwenda na huwa mahitaji nayo yanaendana na wale wanaotoka huku nyuma, wanaotoka awali kwenda darasa la kwanza, wanaotoka darasa la saba kwenda Form One. Kwa hiyo, kila mwaka Serikali inaendelea kufanya tathmini na maoteo ya wale ambao wanamaliza na kuona ni namna gani ambavyo fedha inaweza ikapatikana kwa ajili ya kuondoa upungufu huu wa madarasa.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kuhusu maboma ya majengo ya Nyumba za Walimu na Madarasa yaliyotelekezwa?

Supplementary Question 2

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Suala la nyumba za walimu ni la kila watumishi, hasa kada yetu ya watendaji wa kata ambao wako vijijini kabisa na wakati mwingine maisha yao huwa hayana usalama wa kutosha. Je, Serikali ina mkakati gani kuwajengea nyumba za kuishi hawa watendaji wa kata?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itafanya tathmini juu ya mahitaji ya nyumba za watendaji wa kata kote nchini, kama ambavyo amesema Mheshimiwa Janejelly na kisha kuona ni bajeti ya kiasi gani inahitajika kwa ajili ya kuweza kujenga nyumba hizi.