Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 131 2024-02-08

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:-

Je, Serikali inafahamu kuna upungufu kiasi gani wa Walimu katika Halmashauri ya Mkalama na ina mpango gani kupunguza pengo hilo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2022 Serikali iliajiri Walimu 9,800 nchi nzima na Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ilipangiwa walimu wa ajira mpya 70, kati ya hao walimu 52 wa shule za msingi na 18 kwa shule za sekondari. Kwa mwaka 2023 Serikali iliajiri walimu 13,130 na Halmashauri ya Mkalama ilipangiwa Walimu 92, kati yao walimu hao, 65 kwa Shule za Msingi na 27 kwa Shule za Sekondari. Serikali inatambua mahitaji ya walimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama na maeneo mengine. Hata hivyo, kila mwaka Serikali inaendelea kupunguza mahitaji ya walimu katika sekta ya elimu na hivi karibuni Serikali itatangaza ajira za walimu baada ya taratibu za kibali kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi kukamilika na kadri ya upatikanaji wa fedha.