Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, Serikali inafahamu kuna upungufu kiasi gani wa Walimu katika Halmashauri ya Mkalama na ina mpango gani kupunguza pengo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa upungufu wa walimu Mkalama bado ni mkubwa sana, Serikali inasema nini kuhusu upendeleo maalum kwa Mkalama kwa mgawo unaofuata wa walimu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, watumishi wote wa umma tayari wapo wale wanaofariki na wale wanaostaafu, tayari wapo kwenye ikama ya kibajeti ya Serikali. Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuziba mapengo yote yanayoachwa na watumishi hawa badala ya kusubiri zile ajira ambazo Rais anatupatia kila mwaka? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack; la kwanza, la upungufu mkubwa wa walimu Mkalama:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwishasema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali iko mbioni kuajiri, ajira mpya za walimu hivi karibuni zitatangazwa na baada ya mchakato huo kukamilika, Serikali itaweka kipaumbele katika maeneo ya pembezoni, ikiwemo jimboni au Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kule anakotokea Mheshimiwa Francis Isack. Kwa hiyo, nikutoe mashaka katika hizi ajira mpya bado utaendelea kupata mgawao wa walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili, hili la vifo, uhamisho na ile mishahara inayobaki; kwa mujibu wa Kanuni B.4(1) – (2) ya Standing Order ya mwaka 2009 ya Utumishi wa Umma, mshahara ule upo katika bajeti ya mwaka husika kwa sababu mshahara ni cash budget. Sasa, mwajiri akichelewa kuomba kibali cha ajira mbadala, ule mshahara unakuwa haupo carried forward kwenye mwaka mwingine wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwatake sasa waajiri, pale wanapopata kifo katika maeneo yao ya halmashauri zao, kwa maana kuna mwajiriwa wake mmoja amefariki au amehama, waombe vibali vya ajira mbadala mara moja ili sisi tuweze ku-compile maombi yote yale na kuyapeleka kwa wenzetu wa Ofisi ya Rais, Utumishi, kuweza kupata vibali vya ajira mbadala, ndani ya mwaka wa fedha husika kama Standing Order ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2009 inavyotaka.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, Serikali inafahamu kuna upungufu kiasi gani wa Walimu katika Halmashauri ya Mkalama na ina mpango gani kupunguza pengo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka walimu katika Jimbo la Singida Mashariki, Wilaya ya Ikungi pamoja na shule za sekondari Lighwa, Mang’onyi, Shule ya Msingi Mbughantigha, Choda, kote? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka walimu kule Singida Mashariki mara baada ya mchakato huu wa ajira mpya kukamilika na Singida Mashariki na maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Nusrat kama Ikungi na mengineyo watapata nao mgao wa walimu hao wapya.