Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 135 2024-02-08

Name

Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti matumizi mabaya ya Akili Mnemba, kutumia Akili Mnemba kuchangia ukuaji wa uchumi nchini?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq Salim Turky, Mbunge wa Mpendae, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya akili mnemba yameendelea kuongezeka siku hadi siku hapa nchini katika kuweka mazingira wezeshi ya matumizi ya akili mnemba, Serikali imechukua jitihada za kutosha kujenga uwezo wa wataalam na kuandaa miongozo ya kisera na kisheria ambayo italinda na kuchochea matumizi sahihi na salama ya teknolojia zinazoibukia ikiwemo akili mnemba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa tayari Serikali imetoa ufadhiri wa masomo ya muda mrefu na muda mfupi kwa watumishi wa umma 500 kwenye maeneo ya teknolojia zinazoibukia ikiwemo eneo la matumizi ya akili mnemba. Kati ya watumishi 500, watumishi 20 tayari wameanza masomo ya kozi ya muda mrefu na nafasi 480 zilizobaki tayari Serikali imetangaza nafasi hizo na mchakato wa kupokea maombi unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imeanza taratibu za ujenzi wa chuo mahiri cha TEHAMA kitakachojengwa Nala Dodoma kwa lengo la kuzalisha wataalam watakokidhi mahitaji yaliyopo kwa sasa ikiwemo hitaji la akili mnemba. Ujenzi wa chuo hiki unaenda sambamba na ujenzi wa vituo vya ubunifu vinane kwenye maeneo ya Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza, Tanga, Mbeya, Arusha, Lindi pamoja na Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha Wizara imeboresha sera ya TEHAMA ya mwaka 2016 kwa kuandaa rasmu mpya ya sera ya mwaka 2024 ambayo itajumuisha maeneo ya akili mnemba. Sambamba na hilo Wizara imekamilisha mkakati wa miaka 10 ya uchumi wa kidigiti unaoainisha maeneo muhimu ya matumizi ya akili mnemba katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa kidigitali. (Makofi)