Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti matumizi mabaya ya Akili Mnemba, kutumia Akili Mnemba kuchangia ukuaji wa uchumi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza niipongeze Serikali kwa hatua hizi ambazo imeanza kuzichukua kwa ajili ya kufanikisha kupata watumishi lakini kupata vyuo ambavyo vitasaidia kwenye kuhakikisha kwamba suala la artificial intelligence kwa maana ya akili mnemba linapewa nafasi yake na umakini wake katika nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni moja tu, kwa wakati huu ambao Taifa letu na dunia imekuwa ikipitia changamoto zinazotokana na mambo ya artificial intelligence, tumeona kuna viongozi na tumeona kuna watumishi na watanzania na watu mbalimbali wakichafuliwa kwa kutumia teknolojia hii. Ni upi mkakati wa Serikali wa haraka ili watanzania wengi wapate elimu kuhusu hili jambo kabla ya madhara makubwa hayajawa especial kwa wakati huu ambapo Taifa linaelekea kwenye uchaguzi watu wasije wakatumia kitu hiki kuendelea kuchafua watu na baadaye wakakosa haki zao za kimsingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni upi mkakati wa Serikali? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali kama ambavyo nimejibu katika majibu ya msingi ni suala la kisera na la kisheria. Hata nchi za G7 mwaka 2018 kule Quebec walikaa na kutathmini kuona madhara makubwa yatakayo sababishwa na artificial intelligence kwa Kiswahili akili mnemba au unaweza ukasema akili bandia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili mwaka 2018 walipitisha baada ya IMF kutoa taarifa ya madhara makubwa katika upande wa cyber financial analysis ambayo ilisababisha upotevu wa fedha takribani dola bilioni 100 mpaka dola bilioni 250. Sasa baada ya kugundua hilo ikabidi wapitie sera zao na sheria ili wajue kwamba hili kosa litatambulika vipi na ili tuchukuwe hatua gani za kisheria kwa sababu huwezi ukachukua, huwezi ukasema kwamba hili ni kosa bila ya kuliweka kwenye sera na bila kuliweka kwenye sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua zipi ambazo tunazichukua kama Serikali za dharura kuhakikisha kwamba Watanzania wanajua ili wasiingie kwenye changamoto hizo. Kazi kubwa ambayo inafanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, tunaanzisha mkakati wa kutoa elimu kwa umma ili waweze kutambua madhara ambayo yanaweza yakatokana na akili mnemba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, akili mnemba ina offensive na ina defensive. Tunachokifanya ni kuhakikisha kwamba tunawapa elimu kuhusiana na offensive side isije ikaleta madhara kwao. Kwa hiyo, huo ndiyo mkakati mkubwa ambao lakini unaenda sambamba sasa na kuhakikisha kwamba tunaisuka sera yetu ya TEHAMA ya mwaka 2016 ikiunganisha na teknolojia zingine zinazoibukia ikiwemo akili mnemba. Kuna internet offence, kuna big data analysis lakini pia kuna cyber security haya yote lazima tuyaweke kwenye sera yetu ili tukaweke sheria ambazo zitatusaidia kuchukua hatua stahiki. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti matumizi mabaya ya Akili Mnemba, kutumia Akili Mnemba kuchangia ukuaji wa uchumi nchini?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Serikali ina mpango gani wakupunguza upotevu wa fedha za mitandaoni kwa kutumia akili mnemba? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi, katika jibu langu la msingi. Serikali ipo katika mkakati wa kuboresha sera yake pia tunatengeneza miongozo ambayo itasaidia kwa sababu artificial intelligence inaweza ikatumika kwenye cyber security, artificial intelligence inaweza ikatumika kwenye big data analysis, artificial intelligence inategemea ni matumizi gani ambayo wewe unayahitaji. Serikali tunaenda kuyaangalia katika upana wake na kuyaweka kwa pamoja ili tuhakikishe kwamba artificial intelligence ikatumike kwa faida na siyo kwa kuleta madhara. Ahsante sana. (Makofi)