Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 136 2024-02-08

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza Mgogoro wa Shamba la Gereza la Mollo – Rukwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika miaka ya nyuma kabla ya mwaka 2018 kulikuwepo na mgogoro wa mipaka ya ardhi kati ya gereza la kilimo Mollo na vijiji vya Msanda, Muungano, Malonje, Songambele na Sikaungu vinavyopakana na gereza hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikao cha Tarehe 24 mwezi Novemba 2023 kilichowahusisha Mheshimiwa Jerry William Silaa, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na wataalamu wa ardhi kilimaliza mgogoro uliyokuwepo kati ya Gereza la Mollo na vijiji husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumaliza mgogoro huu ilikubalika na pande zote kwamba Jeshi la Magereza libakie na eneo lenye ukubwa wa ekari 8,989.4 na vijiji vibakie nae neo lenye ukubwa wa ekari 1,800. Baada ya makubaliano hayo Jeshi la Magereza lilipima na kubainisha mipaka ya eneo lake huku vijiji pia vikitambua maeneo yao. Hivyo kwa sasa hakuna mgogoro tena baina ya Gereza la Mollo na vijiji vinavyopakana nalo. Ahsante. (Makofi)