Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 12 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 196 2024-02-14

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: -

Je, Serikali inafanya nini kuhakikisha Miradi ya TASAF inakuwa yenye tija kwa wanufaika?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango wa TASAF unatekelezwa ukiwa na dhumuni kubwa la kuzikwamua kaya zisizojiweza kiuchumi ili ziweze kumudu kukabiliana na changamoto za kiuchumi kupitia afua mbalimbali kama vile uhawilishaji fedha, uundaji wa vikundi vya kuweka akiba na kuinua uchumi wa kaya na utekelezaji wa miradi ya ajira za muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa miradi ya TASAF inakuwa yenye tija kwa wanufaika wake, Serikali imeweka mifumo na mikakati mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Mchakato wa uteuzi kuwa shirikishi na jumuishi, kuweka mfumo wa uwajibikaji na Ufuatiliaji, Utoaji wa taarifa za utekelezaji, kuwapa wanufaika mafunzo ya kuwajengea uwezo, kushirikisha wadau mbalimbali katika ngazi zote za kuhakiki taratibu na miongozo kwenye utekelezaji ikizingatiwa ili kufika ubora, pamoja na hilo pia, viwango na tija inayokusudiwa viangaliwe.