Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, Serikali inafanya nini kuhakikisha Miradi ya TASAF inakuwa yenye tija kwa wanufaika?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na nia nzuri ya Serikali juu ya TASAF kumekuwa na changamoto nyingi sana, miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na kwamba pesa wanazostahili kulipwa wasimamizi na waratibu hazipelekwi au hazipatikani, lakini pia hata kama zikienda zinaenda kwa muda uliochelewa, semina ambazo ndiyo stahiki zitakazowesha kufanyika kwa jambo hili hazifanyiki kabisa; je, ni lini Serikali itatatua changamoto hizi?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu changamoto ambazo Mheshimiwa Mbunge amezieleza nataka kukuhakikishia kwamba kwangu mimi kama Waziri mhusika tunazichukua na kwenda kuzifanyia kazi, lakini nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako, miongozo iliyotolewa kwa ajili ya kufanyika kwa hizi zote ambazo amezisema Mheshimiwa Mbunge ipo wazi, kwa mfano, kwa upande wa semina, upande wa semina fedha zinafika ndani ya muda kama Lulindi au Wilayani kwao hazijafika fedha hizi, basi mimi naomba nizungumze na Mheshimiwa Mbunge ili anieleze, lakini sio yeye tu pamoja na Wabunge wengine ambao wana matatizo kama haya nao pia nitapenda wanifuate nipate taarifa zao ili sasa tuweze kuwasimamia wenzetu wa TASAF ili mambo hayo yaweze kwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka nikuhakikishie kuwa Serikali imepeleka hela nyingi za kutosha, kama uzembe upo ni kwenye usimamizi ambao sisi kama Serikali hatutoufumbia macho.