Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 12 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 200 2024-02-14

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya viwanja vilivyouzwa na Halmashauri ya Wilaya Kibaha eneo la Kisabi na baadae kuzuiwa kuviendeleza?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Kibaha ilisanifu na kutekeleza mradi wa upimaji viwanja katika Eneo la Kisabi mwaka, 2010. Jumla ya viwanja 262 vya matumizi mbalimbali ya ardhi vilipimwa na kusajiliwa kupitia ramani za upimaji namba E1359/378, E1359/379, E1359/382 na E1359/383. Viwanja hivyo viliuzwa na kugawiwa kwa waendelezaji mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2021 Taasisi ya Taifa ya Kusimamia Mazingira (NEMC) ilisitisha uendelezaji wa viwanja hivyo kutokana na viwanja hivyo kupimwa kwenye Bonde la Mto Ruvu kwa kuwa uendelezaji wake ungeathiri bayoanuai katika eneo hilo. Kufuatia hali hiyo, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira kupitia barua ya tarehe 18 Aprili, 2022 iliagiza Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kufanya Tathmini ya Mazingira ya Kimkakati ili kubaini athari za kimazingira zinazoweza kujitokeza kutokana na uendelezaji huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suluhisho la kudumu la suala hili litapatikana baada ya kufanyika kwa tathmini hiyo ambayo inatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2024/2025.