Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya viwanja vilivyouzwa na Halmashauri ya Wilaya Kibaha eneo la Kisabi na baadae kuzuiwa kuviendeleza?

Supplementary Question 1

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Iwapo tathmini hii itakapo kuwa imekamilika na ikagundulika kwamba wananchi wale hawatoweza tena kujenga katika eneo hilo kutokana na sababu za kimazingira; je, Serikali itakuwa tayari kuwafidia wananchi hao kutokana na hali halisi ya thamani ya ardhi ilivyo hivi sasa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, pale kwenye Jimbo la Kibiti, kwenye Kata ya Dimani kuna mwekezaji ambaye anaitwa Carbon Planet. Mwekezaji yule amechukua ardhi takribani hekari 20,000 na ameshaanza kuitumia. Hivi sasa ninavyozungumza ni miaka 20 imeshapita na valuation imeshafanyika lakini wananchi wale bado hawajalipwa kwa kisingizio kwamba, mpaka mwekezaji apate title deed. Nataka commitment ya Serikali. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuambatana na mimi kwenda Kibiti pale Dimani, kuzungumza na Wananchi wa Ngulakula pamoja na Milagha kuhusiana na kadhia hii? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naanza na swali la kwanza la fidia. Ni utaratibu wa kawaida kabisa, itakapobainika kwamba kuna athari ambazo zimewazuia wananchi wale kutoendeleza maeneo yao ambayo walikuwa wamekwishapewa, Serikali itachukua hatua za kuangalia uwezekano wa kupata fidia katika maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali hili la pili la Mheshimiwa Mpembenwe, eneo hili ambalo limechukuliwa na Watu wa Carbon Planet ambao wamekaa pale kwa miaka 22 na wana ekari takriban 20,000; na Mheshimiwa Mbunge ameomba mimi nifuatane naye. Mheshimiwa Mbunge, nakupa uhakika kwamba niko tayari kufuatana na wewe kwenda kukutana na wananchi lakini kuangalia athari ambayo imewapata wananchi hawa na kuona namna tutakavyoweza kumaliza tatizo. (Makofi)

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya viwanja vilivyouzwa na Halmashauri ya Wilaya Kibaha eneo la Kisabi na baadae kuzuiwa kuviendeleza?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Ninataka kuuliza kwamba, hasara zinazosababishwa na watumishi wa Serikali ambao wanagawa viwanja mara mbili mbili au kama hivyo wamekosea designing na kwenda kwenye maeneo ambayo kibioanuwai hayakubaliki; zinafidiwa na nani?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hasara yoyote ambayo inasababishwa na watumishi wa Serikali, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali dhidi ya hawa wanaosababisha hasara hizi. Kumekuwepo na hatua mbalimbali za kuchukua tahadhari lakini kuwafidia wale waathirika; kwa sababu katika mazingira ya kawaida, watu waliopewa kiwanja kimoja katika eneo moja, tunaona uwezekano wa jinsi ya kuwafidia kwa sababu tumeelekeza halmashauri zote nchini kuwa na akiba ya ardhi ili kutatua migogoro hii kwa kuwapa viwanja vingine mbadala wale wote watakaobainika kuwa wamepewa double allocation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua kali zimechukuliwa. Kwa mfano hapa Dodoma kuna idadi kubwa tu ya watumishi tumewapeleka kwenye vyombo kuangaliwa utendaji kazi wao mbovu ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya viwanja vilivyouzwa na Halmashauri ya Wilaya Kibaha eneo la Kisabi na baadae kuzuiwa kuviendeleza?

Supplementary Question 3

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kumekuwa na utaratibu wa Serikali, kwamba wananchi wa eneo fulani hawawezi kupata hati hadi wananchi wote wa eneo lile pale waweze kulipia na wakamilike. Mathalani, eneo kama la Matamba na Tandala – Makete watu wamelipia tangu mwaka 2019 lakini hawawezi kupata hati hadi wananchi wote wa eneo husika waweze kulipia.

Je, Serikali haioni kwamba utaratibu huu unakwamisha jitihada za wananchi kupambana na kupata hati ili waweze kuendeleza makazi yao?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba nijibu swali dogo la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la msingi kwenye eneo hili la hati kwa vile vijiji, actually kilichotokea pale ni zile kampuni za urasimishaji ambazo zilipewa kazi na katika utaratibu wao wa kulipana katika kuendelesha shughuli za gharama za kupima vile viwanja hapo ndipo jam ya kwanza ilipoanzia. Walikuwa wamekubaliana kwamba, watakapolipa wale wote ndipo zoezi lile lifanyike kwa ujumla wake halafu hati zitolewe. Sasa waliolipa ni asilimia ndogo sana ambayo yule mkandarasi ameshindwa kuendeleza ile kazi ya ujumla ya kubaini yale maeneo, na hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa sana. Wizara tumechukua tahadhari ya kutosha, na sasa tunapitia kila kampuni kuona uwezekano wa wale waliolipia tayari waweze kutendewa haki wao kwa sababu wanasubiri hati hizo kwa karibu. Mheshimiwa Sanga tutawasiliana ili kuona ni kampuni gani ilikuwa kwenye eneo lako ili tuweze kutoa mwelekeo ulio sahihi. (Makofi)