Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 202 2024-02-14

Name

Mustafa Mwinyikondo Rajab

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza: -

Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Maungani – Dimani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mustafa Mwinyikondo Rajab, Mbunge wa Dimani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Maungani kilichopo Dimani ulianza mwaka 1990 kwa kutumia nguvu za wananchi. Ujenzi huo ulisimama ukiwa umefikia hatua ya lenta kwa kukosa fedha na kiasi cha shilingi 30,000,000 zilikuwa zimetumika. Tathmini ya kumalizia ujenzi huo ili kuunga mkono nguvu na jitihada za wananchi imeshafanyika na kiasi cha fedha shilingi 108,000,000 kinahitajika. Fedha hizo zitatengwa kwenye mpango wa matumizi ya mfuko wa Tuzo na Tozo kwa mwaka 2024/2025, nashukuru. (Makofi)