Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mustafa Mwinyikondo Rajab

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza: - Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Maungani – Dimani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kituo hiki kimejengwa kwa muda mrefu hivi sasa na kwa kuwa katika eneo hili kuna wananchi wamezunguka na sasa hivi wameshaanza ujenzi;

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana nami kwenda kuhakiki mipaka ya ukubwa wa eneo hili? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na napenda kumueleza Mheshimiwa Mbunge kuwa niko tayari. Tutaongozana ili kwenda kutatua tatizo la mipaka lililopo, ahsante sana.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza: - Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Maungani – Dimani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kinipa fursa na mimi kuuliza swali la nyongeza. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Nyamhongolo katika Manispaa ya Ilemela walitoa eneo la square meter 6,339 kwa ajili ya kujenga miundombinu ya kituo cha polisi zikiwemo nyumba 12 pamoja na kituo chenyewe. Tayari nyumba sita zimekamilika na askari wapo, nyumba sita hazijakamilika na kituo kimefikia asilimia 75 kwa nguvu za wananchi.

Je, ni lini Serikali sasa itakamilisha miundombinu hiyo ili kituo hicho cha polisi kiweze kuanza kazi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mabula, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza kwa namna ambavyo anavyofuatilia kwa karibu na kuhakikisha kwamba ujenzi wa kituo kicho unakamilishwa. Kwa kweli kwa maendeleo makubwa yaliyofanyika katika Wilaya ya Ilemela, hasa kwa kuwa kituo hiki kiko karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Nyamhongolo; ni kipaumbele chetu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Jeshi la Polisi kukipa fedha ili kiweze kukamilika. ninamwahidi Mheshimiwa, tutafuatilia maelekezo tuliyoyatoa ili ujenzi wa kituo hicho ukamilishwe, ahsante.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza: - Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Maungani – Dimani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kilindi haina ofisi au kituo cha polisi na Wizara imekwishaahidi zaidi ya mara tano. Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya Mambo ya Ndani amekwishafika Wilaya ya Kilindi na kujionea ambavyo mazingira siyo mazuri. Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, naomba kupata kauli yako.

Ni lini mtajenga kituo cha polisi katika Wilaya ya Kilindi? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kipaumbele cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuhakikisha kwamba maeneo yote ya Mikoa na Wilaya ambayo hayana Vituo vya Polisi kwa ngazi hizo wanajengewa vituo hivyo. Nikupe assurance Mheshimiwa Kigua, kwamba Wilaya yako ya Kilindi, ni moja ya Wilaya itakayopewa kipaumbele mara tutakapopata fedha za maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Ngazi ya Wilaya, hasa kwa kuzingatia kwamba umepata wahamiaji wengi kutoka kule Ngorongoro na ni wafugaji wanahitaji kuwa na Kituo cha Polisi chenye hadhi hiyo ili waweze kuhudumiwa ipasavyo. Ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza: - Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Maungani – Dimani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Kanda Maalum ya Kipolisi ya Tarime - Rorya, ina Wilaya za Kipolisi za Sirari, Nyamwaga, Tarime, Utegi, Shirati na Kinesi ambazo havina hadhi ya Vituo vya Polisi vya Wilaya kwa sababu kwanza zimejengwa muda mrefu na ni chakavu.

Je, ni lini Serikali inaenda kujenga vituo hivi vya Kipolisi vya Wilaya kwa hadhi ya kisasa kama tunavyoona kwenye Wilaya za Kipolisi, kwenye Mikoa mingine? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa swali la Mheshimiwa Esther Matiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani angeanza kuishukuru Serikali kwa kujenga Kituo cha kisasa kabisa cha ngazi ya Mkoa pale Tarime Mjini. Sasa tulisema baada ya kumaliza kujenga Kituo cha ngazi ya Mkoa, hatua itakayofuata ni kujenga ngazi ya Wilaya, nikuondoe shaka Mheshimiwa Matiko, mara tutakapopata fedha kwa ajili ya maendeleo tutazingatia Wilaya zako kwa kipaumbele ambacho tutakubaliana na Wabunge wa maeneo hayo. Ahsante.