Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2024-02-05

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-

Je, ni hatua gani zimechukuliwa kwa Halmashauri zisizonunua mafuta ya watu wenye Ualbino?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwezesha upatikanaji wa mafuta kwa watu wenye Ualbino kupitia Halmashauri kote nchini. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 na 2022/2023 jumla ya Halmashauri 41 zilitenga na kununua mafuta kinga yenye thamani ya shilingi milioni 47 na kuyagawa kwa wahitaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeelekeza halmashauri ambazo hazikutenga bajeti na kununua mafuta ya watu wenye Ualbino kuzingatia maelekezo ya Serikali yaliyotolewa kupitia Barua Kumb.Na. AB.24/227/01/63 ya tarehe 8 Agosti, 2021, ahsante.