Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 207 2024-02-14

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara kutoka Njiapanda/Ikungu kwenda Malampaka kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Ikungu kwenda Malampaka yenye urefu wa kilometa 15 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa jumla ya kilometa 2.9 zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, Mkandarasi anaendelea na ujenzi wa kilometa 1.7 na kazi inategemewa kukamilika mwezi Juni, 2024. Kwa sehemu iliyobaki yenye urefu wa kilometa 10.4, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi, ahsante.