Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara kutoka Njiapanda/Ikungu kwenda Malampaka kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utaratibu ambao Serikali inaueleza, ina maana itachukua miaka sita kumaliza kipande cha barabara kilichobaki. Naelewa subira inavuta heri, lakini kwenye hii barabara subira inavuta balaa. Je, Serikali haioni kuna umuhimu sasa wa kutenga bajeti ya kutosha mwaka wa fedha ujao ili barabara hii kwa umuhimu wake iweze kujengwa kwa lami kwa muda wa mwaka mmoja ujao? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Mbunge wa Maswa Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari maelekezo yameshatolewa, kipande hiki kwanza nisanifiwe chote kwa sababu utaratibu ulikuwa unafanyika ni sanifu, jenga. Kipande chote kitafanyiwa usanifu. Tunatambua kwamba Malampaka kitakuwa ni moja ya vituo vikubwa vya kati vya SGR ambapo ndiyo mizigo mingi itakuwa inatoka kwenda miji ya Bariadi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tayari Serikali imeshaliona hilo na tumeelekeza wafanye usanifu ili tuweze sasa kukijenga kipande chote kwa standard ya kubeba mizigo yote mikubwa kutoka kituo cha SGR cha Malampaka, ahsante. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara kutoka Njiapanda/Ikungu kwenda Malampaka kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tunafahamu kwamba barabara ya kutoka Malagarasi kwenda Uvinza inaendelea kujengwa, lakini kwa wakati huu ambapo mvua zinaendelea kunyesha wananchi wanaendelea kupata shida kwenye kipande kile cha kilometa 50 kutoka Uvinza mpaka Malagarasi. Je, ni lini barabara hiyo ya kutoka Malagarasi mpaka Uvinza itakamilika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Kigoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kigoma kuna mvua nyingi tunatambua, lakini mkandarasi yupo anafanya kazi katika kipande hicho cha Malagarasi hadi Uvinza. Kwa hiyo, kinachokea ni kwamba, kwenye zile barabara za bypass, zile diversion ambazo najua Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba eneo la Kigoma na hasa lile eneo ni udongo wa mfinyanzi mkali sana, kwa hiyo, labda tu nimpe maelekezo Meneja wa Mkoa wa Kigoma kuhakikisha kwamba barabara zile za divertsion zikarabatiwe vizuri ili magari yaendelee kupita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kukamilika kwa hiyo barabara, Mheshimiwa Mbunge anafahamu Mkandarasi yupo site, na kwa sasa kwa sababu ya hali hii ya mvua, wakandarasi wengi wameshindwa kufanya kazi kwa kasi, kwa sababu katika kipindi cha mvua ni ngumu sana kufanya kazi hasa za kushindilia udongo kwa sababu unakuwa umelowa. Kwa hiyo, lazima tusubiri mpaka kipindi cha mvua kitakapokuwa kimepita tutahakikisha tunamsimamia ili aweze kukamilisha hiyo barabara kwa haraka sana, ahsante.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa barabara kutoka Njiapanda/Ikungu kwenda Malampaka kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Jimbo la Busokelo na Rungwe wanataka kujua, je, ni lini barabara ya kuanzia Tukuyu Mjini – Mbambo - Mwakaleli – Suma kutokea Katumba pale maarufu kama Kikuba itakamilika? Barabara hii ni kiunganishi kikubwa sana, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara hii ilishaanza kujengwa, lakini kuna vipande ambavyo bado havijakamilika. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya kwamba tayari tupo kwenye hatua za mwisho za vipande vile vilivyobaki ambavyo vimegawanywa katika lot mbili ku-sign ili mkandarasi sasa aweze kupewa na kuendelea na hiyo kazi ya kukamilisha vile vipande viwili ambavyo vimebaki. Kwa hiyo, tupo kwenye hatua za mwisho kabisa ili tuweze ku-sign kwa sababu mkandarasi alishapatikana, ahsante.