Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2024-04-15

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha hadhi Zahanati za Madope na Ludende kuwa Vituo vya Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Zahanati za Madope na Ludende ni zahanati zilizopo kwenye Makao Makuu ya Kata za Madope na Ludende mtawalia. Zahanati ya Madope ina eneo la takribani ekari 10, pamoja na vigezo vingine, inakidhi kuwa kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Ludewa itatenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuongeza majengo na kuanza utaratibu wa kuipandisha hadhi Zahanati ya Madope kuwa kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Zahanati ya Ludende haikidhi vigezo vya kuwa kituo cha afya kwa kuwa, ina eneo dogo na uchache wa watu na pia, inapakana na Kituo cha Afya cha Mlangali na vingine. Ahsante.