Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 6 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 71 2024-04-15

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:-

Je, lini Serikali itafanyia kazi changamoto ya Kodi na Tozo kwenye Fedha za Mfuko wa Jimbo kwa upande wa Zanzibar?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Jimbo la Wingwi kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kodi na tozo hutozwa kwa mujibu wa Sheria pindi bidhaa au huduma zinapotolewa au kununuliwa. Aidha, bidhaa na huduma zinazotolewa hukatwa kodi ya zuio la kodi (withholding tax) kwa kuzingatia Sheria ya Kodi ya Mapato, Sura ya 332, chini ya Kifungu cha 83(1)(c) kwa mujibu wa ada ya huduma kwa ajili ya utoaji wa huduma za kitaalam. Aidha, Kifungu cha 83A, malipo ya bidhaa zinazotolewa na mkazi wa uendeshaji biashara. Vilevile, kodi hutozwa kwa kuzingatia Sheria ya Manunuzi iliyotumika Zanzibar inayojulikana kama Sheria zinazotolewa na mkazi wakati wa uendeshaji wa biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za Mfuko wa Jimbo zinaendelea kuleta tija na matokeo chanya katika kuimarisha na kukuza uchumi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla na hivyo huleta manufaa kwa wananchi wa pande zote mbili za Muungano. Nakushukuru.