Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itafanyia kazi changamoto ya Kodi na Tozo kwenye Fedha za Mfuko wa Jimbo kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini kabla sijauliza naomba kusahihisha, ni Mkoa wa Kaskazini Pemba, Wilaya ya Micheweni, siyo Mkoa wa Kaskazini Unguja. Sasa, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza Sheria mbalimbali ambazo zinakata kodi kwa Mfuko huu wa Majimbo kwa upande wa Zanzibar, ikiwemo upande wa Jamhuri na ile ya upande wa Serikali ya Zanzibar. Je, Serikali zote mbili hazioni haja ya kukaa pamoja na kuona namna ya kupunguza au kuondoa kabisa kodi hizi kwa ukizingatia kwamba, mifuko hii inakwenda kuwahudumia wananchi moja kwa moja?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, Serikali haioni haja ya kutoa maelekezo kwa Halmashauri za Zanzibar kwamba, wasitumie fedha hizi kama vyanzo vyao vingine vya mapato ya halmashauri kwa vile fedha hizi vilevile zinawahudumia wananchi wa Zanzibar kwenye majimbo yetu? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kombo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka Waheshimiwa Wabunge wote wafahamu kwamba, makato ya fedha hizi yapo kisheria, yanakatwa kwa mujibu wa Sheria. Maana yake ni kwamba, uwepo wa hizi kodi ni kwa sababu, Sheria zipo na zinawaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri, wa Majiji, wa Mabaraza ya Miji kwamba, fedha hizi zinazotumika kununua vifaa kwa ajili ya Mfuko wa Jimbo ni lazima zikatwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli fedha hizi ni kidogo, lakini zinatumika kwenye miradi ya jamii, mahitaji ya fedha hizi ni mengi uki-compare na zinazotoka. Waheshimiwa Wabunge, ni lazima tukubaliane kwamba, fedha hizi ni lazima zikatwe kodi, ili halmashauri zetu ziweze kupata kipato.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine ninachotaka kuwaambia Waheshimiwa, ni tumefanya vikao mara kadhaa na Waheshimiwa Wabunge, Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri, wa Majiji, wa Mabaraza ya Miji na taasisi zinazokusanya fedha, zikiwemo ZRA na ZRB, lengo na madhumuni ni kuona namna ambavyo tunawaelimisha Waheshimiwa Wabunge na wengine ili waweze kufahamu hilo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, mweleze kwa kifupi.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba, kama alivyoshauri basi tutalichukua na kwenda kuyafanyia kazi yale ambayo ameshauri.