Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 73 2024-04-15

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:-
Je, lini barabara ya Gomvu - Kimbiji – Pembamnazi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Gomvu – Kimbiji – Pembamnazi ni sehemu ya barabara ya Mjimwema – Kimbiji - Pembamnazi yenye urefu wa kilometa 49 ambayo inajengwa kwa awamu kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa sehemu ya Cheka – Avic yenye urefu wa kilometa mbili tayari ujenzi umekamilika. Kwa sehemu ya Avic – Kimbiji kilometa 10 taratibu za manunuzi ya kumpata mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi zinaendelea. Ujenzi kwa sehemu iliyobaki ya Kimbiji hadi Pembamnazi itajengwa kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante sana. (Makofi)