Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Je, lini barabara ya Gomvu - Kimbiji – Pembamnazi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; barabara ambayo ameitoa alipotoka kujibu maswali Mheshimiwa Waziri kutokana na athari za mvua zinazoendelea sasa hivi imekatika na wananchi wanapata shida kubwa sana especially katika maeneo ya kwa Moris na maeneo mengine pale Kimbiji. Je, nini mkakati wa muda mfupi wa ukarabati wa barabara hii ili wananchi wa Pemba Mnazi waweze kufika katika maeneo kwa gharama nafuu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; ni Barabara ya Kibada – Mwasonga. Barabara hii yenye urefu wa kilometa 41 na inatumika kwa magari mengi mazito lakini barabara hii mkataba wake umeshasainiwa mwezi Machi, 2024 na sasa hivi imeharibika sana. Wananchi wa Kigamboni wanataka kujua na kupata kauli ya Serikali ni lini ujenzi wa barabara hii utaanza? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndugulile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ni kuhusu Mvua za El-Nino zinazoendelea na kukatika kwa barabara. Nitumie nafasi hii kuendelea kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa namna ambavyo wameendelea kutupa ushirikiano kwenye majimbo yao pale mawasiliano yanapokatika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru pia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha za emergency ili tuweze kurekebisha pale ambapo mawasiliano yanakatika. Kwa upande wa Mheshimiwa Dkt. Ndugulile nimwelekeze Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Dar es Salaam kufika maeneo haya na kufanya tathmini ili tuweze kujitahidi kwa kadri inavyowezekana kuhakikisha mawasiliano ya barabara yanaendelea kuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la pili kuhusu Barabara ya Kibada – Mwasonga kilometa 47, tunamshukuru pia Mheshimiwa Rais kwa kutupa kibali kwa kusaini baadhi ya barabara ambazo zimefikia hatua ya kusainiwa ili ujenzi uanze. Barabara hii Jimboni kwa Mheshimiwa Ndugulile ni kweli mkandarasi alisaini mkataba huu mwezi Machi na sasa hivi namwelekeza mkandarasi kuendelea na mobilization wakati tukimtafutia taratibu za malipo ya advance. Vilevile, Mkandarasi huyu anawajibika kufanya matengenezo ya barabara kwa sababu tumeshamkabidhi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Je, lini barabara ya Gomvu - Kimbiji – Pembamnazi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi. Barabara ya kutoka Mtama – Kitangali kwenda Newala Jimbo la Newala Vijijini inapitika kwa shida kwa sababu ya ubovu wa barabara ile kwa muda mrefu. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami ili kuwanusuru wananchi wa Newala na hali ambayo ipo? Ahsante. (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Barabara ya Mtama – Newala ni kweli barabara hii Waheshimiwa Wabunge wamekuwa wakiomba muda mrefu kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini niwaombe Waheshimiwa Wabunge tuendelee kuitengeneza barabara hii kwa kiwango cha changarawe. Kwenye vipaumbele vya Wizara ya Ujenzi tutaangalia namna ya kuanza kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana kwa kujenga kwa kiwango cha lami. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Je, lini barabara ya Gomvu - Kimbiji – Pembamnazi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Barabara ya Makofia – Mlandizi – Mlandizi Vikumburu imeshafanyiwa tathmini na wananchi wanasubiri kupata fidia. Je, Serikali imefikia hatua gani ya kuwalipa ili barabara hii iweze kutengenezwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael kuhusu Barabara ya Makofia – Mlandizi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ni kipaumbele kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema, lakini naomba yeye pamoja na wananchi waendelee kuwa na Subira, tutaiweka kwenye vipaumbele kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Je, lini barabara ya Gomvu - Kimbiji – Pembamnazi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni ahadi ya Mheshimiwa Rais kwamba Barabara ya kutoka Bunju B kwenda Mabwepande mpaka Ubungo ijengwe kwa kiwango cha lami. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gwajima, Mbunge wa Jimbo la Kawe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii ni muhimu, lakini Mheshimiwa Gwajima na Waheshimiwa Wabunge kama wanavyofahamu sasa hivi kuna ukatikaji wa mawasiliano ya barabara na madaraja kote nchini, kipaumbele namba moja ni kuhakikisha tunarudisha mawasiliano haya ili shughuli za uzalishaji kiuchumi na kijamii ziweze kuendelea. Kwa hiyo barabara hizi ikiwemo hii barabara ambayo Mheshimiwa Gwajima amekuwa akiifuatilia kwa karibu tumuahidi yeye pamoja na wananchi kwamba kadri fedha zitakavyopatikana na yenyewe tutaiweka kwenye vipaumbele. Ahsante sana. (Makofi)