Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 77 2024-04-15

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Jengo la Makumbusho katika Kijiji cha Nandete ili kuhifadhi kumbukumbu za Vita vya Majimaji?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Ndulane kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa makumbusho unahitaji utafiti wa kina wa historia ya eneo husika ili kuweza kupata taarifa na mikusanyo itakayowekwa kwenye makumbusho tarajiwa. Kwa kutambua umuhimu wa historia ya vita vya Majimaji katika eneo la Nandete, Serikali kwa kushirikiana na wadau imeanza kufanya utafiti kwenye eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na jitihada hizo mwaka 2022 Serikali imefanya maboresho ya Sheria ya Mambo ya Kale, Sura ya 333 ili kuruhusu watu binafsi na taasisi mbalimbali kuanzisha makumbusho binafsi kwa lengo la kuhifadhi na kuendeleza utalii unaohusiana na utajiri wa kihistoria uliopo. Natoa wito kwa wadau wetu kutumia fursa hiyo kujenga makumbusho kwenye maeneo ya kihistoria hapa nchini ili kuendeleza historia na kujipatia kipato.