Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Jengo la Makumbusho katika Kijiji cha Nandete ili kuhifadhi kumbukumbu za Vita vya Majimaji?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kupata jibu zuri linaloashiria uendelevu wa kumbukizi hizi. Pia napenda kuipongeza Serikali mwezi uliopita tarehe 15 ilitoa GN ya Maadhimisho haya ya Kumbukizi za Majimaji. Kwa hiyo, kwa niaba ya mashujaa 30 walioongoza vita hii pamoja na wananchi wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, naipongeza sana Serikali kwa hatua hii, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa GN imepatikana ya kumbukizi hizi, je, ni lini Serikali itaanza kutenga fedha kwa ajili ya maadhimisho ya kumbukizi hizi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, Serikali ina mkakati gani kwa kushirikisha Wizara ya Maliasili na Utalii, Taasisi ya TARURA na TANROADS kuwezesha barabara zinazokwenda kwenye kumbukizi hizi ziweze kupitika katika kipindi chote cha mwaka mzima? (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepokea pongezi za Mheshimiwa Mbunge. Kama tunavyofahamu tupo kwenye kipindi cha bajeti, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kipindi bajeti ya Wizara hii itakapofika, basi tuweze kuipitisha ili tuweze kufanya haya ambayo yanayoombwa na Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na hili suala la barabara, barabara zote ambazo zipo kwenye maeneo ya hifadhi tunaishukuru Serikali imetupatia vifaa na fedha za kuweza kufanya ukarabati kwenye maeneo haya. Vilevile kama tulivyomsikia Waziri wa Miundombinu muda mfupi uliopita kwamba Serikali imetoa fedha za kuhakikisha inafanya ukarabati kwenye maeneo ambayo yamepata changamoto ili ziweze kupitika. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwa barabara mahsusi ambazo zina tatizo hili, awasiliane na Wizara husika ili ziweze kufanyiwa kazi. (Makofi)