Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 5 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 64 2016-09-13

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA HASSAN TOUFIQ aliuliza:-
Sheria ya Kutambua Haki ya Msaada wa Kisheria (Legal Aid) ambayo pia inawatambua wasaidizi wa kisheria (paralegals) mchakato wake umeanza tangu mwaka 2010 kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo taasisi zisizo za Kiserikali, lakini sheria hii imekuwa ni ya muda mrefu na sasa ni zaidi ya miaka sita bado haijatajwa wala kuletwa Bungeni.
Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha sheria hii inatungwa?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha hatua zote za awali za kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria katika Bunge lako Tukufu. Muswada huo unalenga kuweka utaratibu wa kisheria wa kuratibu huduma ya msaada wa kisheria nchini na kuwatambua Wasaidizi wa Kisheria waliokidhi vigezo mahususi vya ujuzi katika utoaji huduma hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali baada ya kutungwa kwa sheria hii ni kuhakikisha huduma ya msaada wa kisheria inapatikana nchi nzima hususani kwa wananchi walio vijijini na ambao hawana uwezo wa kumudu gharama za Mawakili ambao wengi wao wanaishi na kufanya shughuli za mijini tu.