Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 5 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 85 2024-02-05

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi baina ya Jeshi la Wananchi na Wananchi California Mtaa wa Mbae Mashariki, Mkoani Mtwara?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo linalozungumziwa lipo katika Kikosi cha Jeshi cha 665 kilichopo Naliendele Mkoani Mtwara. Eneo hilo linalokizunguka Kikosi hicho lilivamiwa na wananchi na mwaka 2014 wananchi walifungua shauri Mahakamani wakidai kumiliki eneo hilo. Hukumu ya shauri hilo ilitolewa mwaka 2021 ambapo Mahakama ilitupilia mbali madai hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupitia Bunge lako Tukufu kuwaomba wananchi kuelewa umuhimu wa maeneo ya jeshi kwa maslahi mapana ya ulinzi na usalama wa Taifa na kutoa ushirikiano. Aidha, naomba wananchi walio ndani ya eneo hilo la jeshi waweze kuondoka kwa kuzingatia taratibu na sheria.