Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi baina ya Jeshi la Wananchi na Wananchi California Mtaa wa Mbae Mashariki, Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri, kwa majibu mazuri. Nina swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo hilo tajwa, lina wanajeshi zaidi ya 10 wapo kwenye maeneo hayo na wamejenga nyumba na wana hatimiliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu, ni lini Serikali itakwenda kufuta hati zile, kwa sababu wanajeshi wale wanakuwa wanawapiga wananchi kwenye maeneo mengine na kuwavunjia nyumba ambazo zimejengwa na wanajeshi pale ambazo zina hati kwenye eneo la Jeshi, bado wanaendelea kukaa?



Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni lini Mheshimiwa Waziri tutaongozana kwenda kwenye eneo husika na wewe ukajionee hali halisi ili tuweze kutatua mgogoro huo kidiplomasia. (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa vile Mheshimiwa Mbunge ameomba tuongozane nikaone hali halisi basi haya yote nitayaona tutakapotembelea eneo hilo na nakubaliana kuongozana naye. (Makofi)

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi baina ya Jeshi la Wananchi na Wananchi California Mtaa wa Mbae Mashariki, Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuulizwa swali la nyongeza; je, ni lini Serikali itatatua migogoro iliyopo katika Wilaya ya Nachingwea kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania JKT pamoja na wananchi?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyoeleza huko nyuma Wizara inayo mpango wa miaka mitatu ambayo inaendelea kuutekeleza na katika mpango huo tayari kulikuwa na maeneo yenye migogoro 87 tumekwishatatua migogoro 78. Kwa hiyo, kwa Eneo la Nachingwea bado tunaendelea kulishughulikia na tutaendelea kulishughulikia ili tuweze kukamilisha, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba migogoro hii yote inatatuliwa.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi baina ya Jeshi la Wananchi na Wananchi California Mtaa wa Mbae Mashariki, Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 3

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale kwenye Kata yangu ya Makoko pamoja na Buhare kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya Jeshi la Wananchi pamoja na wale raia wa pale na Waziri aliyekuwepo Mheshimiwa Innocent Bashungwa aliahidi kwenda na mimi kwa ajili ya kwenda kutatua huo mgogoro.

Je, sasa ni lini Mheshimiwa Waziri uliyepo sasa utaandamana na mimi tukamalize huo mgogoro wa wananchi? (Makofi)

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri aliyenitangulia alikwishatembelea eneo hilo na amekwishanipa taarifa kuhusu hatua iliyofikiwa. Kwa hiyo, tunaendelea hapo alipofikia na kama itahitajika twende tena basi tutafanya hivyo, lakini nafikiri tuna imani kwamba kwa ripoti aliyoitoa tutaweza kukamilisha tatizo hili na mgogoro huo, ahsante.