Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 86 2024-02-05

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo ya Chuo cha VETA Namtumbo yakiwemo mabweni, bwalo la chakula pamoja na Lecture Hall?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilitenga na kupeleka shilingi milioni 600 katika Chuo cha VETA cha Namtumbo ikiwa ni bajeti ya awali kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa mabweni mawili moja la wanafunzi wa kiume na moja la wanafunzi wa kike, bwalo la chakula na jiko pamoja na nyumba za watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huo unatekelezwa kwa awamu ambapo kwa awamu ya kwanza ujenzi wa mabweni mawili umefikia hatua ya kuezeka na unatarajiwa kukamilika mwaka huu wa fedha 2023/2024.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu iliyosalia ambayo inajumuisha ujenzi wa nyumba za watumishi, jiko pamoja na bwalo la chakula ambalo litatumika kwa matumizi mbalimbali ikiwamo shughuli za mihadhara, nakushukuru.