Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo ya Chuo cha VETA Namtumbo yakiwemo mabweni, bwalo la chakula pamoja na Lecture Hall?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kwanza kwa ruhusa yako niishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mheshimiwa Rais wetu mpendwa kwa kutuletea fedha nyingi kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya yetu ya Namtumbo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali; kwa kuwa mradi huu wa majengo yale ya mabweni ukikamilika katika Chuo chetu cha VETA utaweka wanafunzi wengi pale katika Chuo cha VETA na watahitaji maji ya kutosha; je, Serikali katika component ya bajeti inayokuja inaweza ikaweka mradi wa kuchimba kisima kwa ajili ya matumizi ya chuo kile pale cha VETA Namtumbo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikalini kuna magari ambayo yamepata ajali yanaweza kutengenezeka Serikalini na Taasisi za Serikali na yanakaa tu bila kufanyiwa maamuzi yanaharibika; je, Serikali inaweza ikafanya uamuzi wa kupeleka katika Vyuo vya VETA yakawa magari hayo ni ya kufundishia wanafunzi wanaofanya ufundi wa utengenezaji magari katika maeneo ya panel beating, urekebishaji wa muundo wa ufundi wa umeme wa magari lakini pia na ufundi wa injini na vifaa vinginevyo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali hasa hasa Serikali hii ya Awamu ya Sita kuhakikisha kwamba huduma zote muhimu zinakuwepo katika vyuo vyetu vile vya zamani, lakini pia hivi vipya ambayo tunavyovijenga.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kwamba tayari Wizara imeshawasiliana na wenzetu wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira kule Namtumbo na UWASA na kuwaomba watuletee bajeti ya uchimbaji wa kisima hicho na tayari wameshatuletea bajeti hiyo ambayo inagharimu shilingi milioni mia moja, laki mbili na arobaini na nane laki tano na sabini na sisi pasipokuwa na shaka tutaweza kuingiza sasa katika bajeti inayokuja 2024/2025 ili wakati majengo haya yakikamilika basi na hiki kisima kiweze kuwa tayari.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili amezungumza suala la magari. Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie na Bunge lako Tukufu kwamba Wizara inayo utaratibu huu, ina utaratibu wa kupeleka magari haya yaliyochakaa, lakini vilevile hata magari mapya na kwa vile amezungumzia habari ya magari hapa utaratibu huo upo na magari haya hupatikana kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo zile za TASAF, TANROADS na taasisi nyingine za Serikali. Kwa hiyo, tutafanya kwa kadri itakavyokuwa imewezekana, nakushukuru.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo ya Chuo cha VETA Namtumbo yakiwemo mabweni, bwalo la chakula pamoja na Lecture Hall?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itapeleka fedha zaidi katika Chuo cha VETA cha Urambo ili tupate majengo zaidi tuongezee stadi zaidi za ufundi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mama Margaret Sitta, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, chuo chetu kile cha VETA, Urambo katika mwaka wa fedha ule uliopita tulipeleka fedha pale kwa ajili ya kuongeza baadhi ya miundombinu lakini vilevile kufanya ukarabati. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Margaret Sitta kwamba katika mwaka huu tena unakuja wa 2024/2025 tutatenga fedha kama tulivyofanya mwaka uliopita kwa ajili ya kuongeza miundombinu lakini vilevile kufanya ukarabati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hii tunaifanya kwa Vyuo vyote pale Urambo tumefanya, lakini Wanging’ombe pale tumepeleka fedha, Newala kule napo vilevile tumepeleka kwa hiyo tutafanya kama tulivyofanya mwaka uliopita wa fedha, nakushukuru sana.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo ya Chuo cha VETA Namtumbo yakiwemo mabweni, bwalo la chakula pamoja na Lecture Hall?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi; je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa bweni la Songwe Girls Secondary School ambayo inachukua wanafunzi wa majimbo sita ndani ya Mkoa wa Songwe?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, hii ya shule na ujenzi wa bweni kidogo naomba nilichukue hili la Mheshimiwa Sichalwe kwa sababu ni ujenzi wa bweni katika shule ya sekondari.

NAIBU SPIKA: Wewe mjibu tu.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru na naomba nijibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna utaratibu wa ujenzi wa mabweni katika shule zetu na tunafahamu kwamba tuna mradi wetu mkubwa sana wa SEQUIP ambao ni mradi ambao una zaidi thamani ya zaidi ya trilioni 1.1.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa vile mgao wa awamu inayofuata bado haujafika nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika ugawaji huo tutazingatia mahitaji ya bweni hilo pale na mimi bahati nzuri nilifanya ziara nikaenda nikaona nimhakikishie kwamba tutajitahidi kuweza kuweka fedha kwa ajili ya ujenzi wa bweni hilo.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa majengo ya Chuo cha VETA Namtumbo yakiwemo mabweni, bwalo la chakula pamoja na Lecture Hall?

Supplementary Question 4

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali imewekeza kwenye ujenzi wa Vyuo vya VETA, lakini kwa uzoefu nimeona masomo mengi yanayotolewa ni yale masomo ambayo ni ya ushonaji, ujenzi na ufundi seremala; lakini ni upi mkakati wa Serikali kuongeza idadi ya masomo yenye soko la sasa kama ufundi wa magari ya umeme, ufundi wa mabomba plumbing na mambo mengine ili iweze kusaidia Watanzania walio wengi na vijana waweze kupata soko kwenye Taifa letu? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru na naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna course zile ambazo ni za general course ambazo katika kila chuo kinatoa, lakini mpango wetu wa sasa kama Serikali tumewaagiza wenzetu wa VETA kuhakikisha kwamba tunakwenda ku-customize zile course kulingana na shughuli za eneo husika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mpango huo tunao na hivi sasa au tuko mbioni kuhakikisha kwamba tunaandaa mitaala ambayo inaendana na shughuli za jamii mahali vyuo vilipo, nakushukuru sana.