Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 137 2024-02-09

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka Walimu wa kutosha katika Shule za Msingi na Sekondari Mkoani Kagera?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benardeta Kasabago Mushashu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2022 Serikali iliajiri Walimu 9,800 na Mkoa wa Kagera ulipangiwa walimu ajira mpya 640. Kati ya hao, walimu 351 wa shule za msingi na 289 kwa shule za Sekondari. Kwa mwaka 2023 Serikali iliajiri Walimu 13,130 na Mkoa wa Kagera ulipangiwa walimu 590, kati yao, walimu 312 ni kwa shule za msingi na 278 ni kwa shule za Sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mahitaji ya Walimu katika Mkoa wa Kagera na maeneo mengine nchini. Hata hivyo serikali kila mwaka inaendelea kupunguza mahitaji ya walimu katika sekta ya elimu; na hivi karibuni Serikali itatangaza ajira za walimu baada ya taratibu za kibali kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi kukamilika na kadiri ya upatikanaji wa fedha.