Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 139 2024-02-09

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa ajira za kutosha kwa Walimu ili kuondoa upungufu uliopo?

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2022 Serikali iliajiri walimu 9,800 wa shule za msingi na sekondari na kwa mwaka 2023 Serikali iliajiri walimu 13,130 wa shule za msingi na sekondari. Serikali inatambua mahitaji ya Walimu kote nchini. Hata hivyo Serikali kila mwaka inaendelea kupunguza mahitaji ya walimu katika sekta ya elimu na hivi karibuni Serikali itatangaza ajira za walimu baada ya taratibu za kibali kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi kukamilika na kadiri ya upatikanaji wa fedha.