Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 140 2024-02-09

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, kwa nini baadhi ya miradi inayoibuliwa na jamii kupitia TASAF hukataliwa na kutekelezwa miradi ambayo haikuibuliwa na jamii?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi yote inayotekelezwa kupitia TASAF huibuliwa na jamii kwa kutumia utaratibu shirikishi unaokutanisha jamii yote katika Kijiji/Mtaa au Shehia katika mkutano wa kuchagua miradi inayoondoa kero za wananchi, inayokubaliwa na jamii na inayokidhi vigezo vya kisekta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, endapo jamii itaibua mradi ambao haukidhi vigezo vya sekta na kuangalia manufaa ya miradi ya kipaumbele cha kwanza kwa jamii, mradi wa pili katika orodha ya vipaumbele vya jamii hutekelezwa.