Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 142 2024-02-09

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: -

Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Kata ya Oldonyosambu ambao maeneo yao yalichukuliwa na Jeshi?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Eneo la Oldonyosambu kuna viteule viwili vya Jeshi ambavyo ni Kiteule cha Kikosi cha Oljoro na Kiteule cha Kikosi cha Rada. Katika maeneo hayo mawili, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa hatujapokea taarifa ya kuwepo kwa maeneo ya wananchi yaliyochukuliwa na Jeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, endapo kuna malalamiko yoyote kuhusu maeneo ya wananchi kuchukuliwa na Jeshi, Wizara ipo tayari kupeleka wataalam katika eneo hili ili kushughulikia malalamiko hayo.