Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 143 2024-02-09

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. AMEIR ABDALLA AMEIR aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani BAKITA na BAKIZA zinaondoa changamoto za matumizi ya Lugha ya Kiswahili Kitaaluma na kijamii?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ameir Abdalla Ameir, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza ya Kiswahili BAKITA na BAKIZA yameendelea kuweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na changamoto za matumizi sahihi ya Kiswahili kitaaluma na kijamii zikiwemo, kuandaa semina za ukalimani; kusanifisha maneno mara tu yanapoibuka kutokana na maendeleo ya Sayansi na teknolojia na ongezeko la matumizi ya mitandao ya kijamii, kutoa elimu ya matumizi fasaha na sanifu ya Lugha kupitia vipindi vya redio na televisheni, kuandaa makongamano ya Idhaa za Kiswahili Duniani kwa lengo la kuelimisha jamii kuhusu matumizi sahihi ya Lugha, kupitia vitabu mbalimbali vilivyoandikwa kwa Kiswahili kwa lengo la kuhakiki usahihi wa Lugha na kutoa ithibati, kuwapiga msasa wataalam wa Kiswahili na kuwapatia mbinu za kufundisha Kiswahili kwa wageni na kusambaza msamiati wa Kiswahili kupitia mitandao ya kijamii.