Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 146 2024-02-09

Name

Maulid Saleh Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: -

Je, Serikali imefikia hatua gani ya kuziunganisha na Mfumo wa NIDA taasisi zote za umma na binafsi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Saleh Ali, Mbunge wa Jimbo la Welezo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mojawapo ya majukumu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ni kuanzisha na kutunza kanzidata ya taarifa za watu na kushirikishana taarifa hizo na taasisi nyingine za umma na binafsi ili kutatua changamoto za utambuzi katika shughuli za kiuchumi, kijamii na kiusalama. Kuanzia mwezi Julai, 2020 NIDA ilipoanza kuunganisha taasisi na kanzidata yake hadi tarehe 6 Januari, 2024 jumla ya taasisi 96 za Serikali na Binafsi zimeunganishwa na kanzidata ya NIDA ambapo taasisi 44 ni za Serikali na taasisi 52 ni za binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa NIDA ni kuendelea kutoa elimu na kuunganisha taasisi 200 ifikapo mwezi Juni, 2026. Kasi ya uunganishaji inatarajiwa kuongezeka kufuatia utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya tarehe 10 Agosti, 2023 ya kutumika kwa namba moja (namba jamii) katika kumtambua mtu wakati wa kumpatia huduma, badala ya mtu mmoja kuwa na namba zaidi ya moja, ahsante.