Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maulid Saleh Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani ya kuziunganisha na Mfumo wa NIDA taasisi zote za umma na binafsi?

Supplementary Question 1

MHE. MAULID SALEH ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Nataka nimuulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; je, Serikali imejipangaje kuweka mahusiano mazuri katika ya NIDA na Jeshi la Polisi katika kutatua taarifa za haraka za mitandao ya kijamii? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, je, Serikali ina uhusiano gani mzuri wa kuhakikisha inatatua matatizo yale ya upelelezi ambayo yanafanyiwa kazi na polisi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kuhusu swali lake la mwanzo, uhusiano kati ya NIDA na Polisi umetengenezwa na tumshukuru Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba NIDA inakuwa chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Polisi ipo chini ya Wizara ya Ndani ya Nchi, chini ya Waziri mmoja, Naibu Waziri mmoja, Katibu Mkuu mmoja. Kwa hiyo, hilo pekee linawakutanisha viongozi wa Taasisi hizi mbili; pale kunapokuwa na changamoto basi hushauriana na kuhakikisha suluhisho hupatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili la uhusiano wa kiupelelezi vilevile panapohitajika huduma za NIDA, kuliwezesha Jeshi la Polisi litimize wajibu wake hasa idara ya upelelezi, ushirikiano hufanyika na hatuishii hapo tu, tunahusiana pia na taasisi nyingine za kiserikali kwa mfano, TCRA ikihitajika pia tupate ushahidi kule kuwezesha Jeshi la Polisi kutimiza wajibu wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani ya kuziunganisha na Mfumo wa NIDA taasisi zote za umma na binafsi?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, katika Jimbo la Hai, wananchi wamekuwa wakipata tabu sana kupata vitambulisho vya NIDA, vinacheleweshwa na sababu kubwa ni kwamba hakuna mashine ya ku-print hivi vitambulisho.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta mashine pale Hai ili wananchi waweze kupata vitambulisho kwa wakati? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mheshimiwa Mafuwe pamoja na Wabunge wengine wote ambao wamekuwa wakihitaji kuona wananchi wao wanapata vitambulisho. Mnakumbuka katika Bunge lililopita na mwishoni mwa mwaka jana kulikuwa na malalamiko ya watu wengi kutopata vitambulisho lakini Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilifanya uamuzi wa makusudi kabisa kutoa fedha za kutosha kuchapisha vitambulisho vyote ambavyo vilikuwa vinahitajika na wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mafuwe, pamoja na kwamba hakuna mashine pale Hai, lakini mitambo iliyoko Dar es Salaam, ina uwezo wa kuchapisha vitambulisho vyote vinavyohitajika kwa wananchi wote kwa muda mfupi sana. Hivi tunavyozungumza vitambulisho vya Wananchi wa Hai vimeshachapishwa, kinachotakiwa sasa ni kuvifikisha kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pengine kama kuna changamoto tutafuatilia kujua hadi sasa kwa nini Wananchi wa Hai wasipate vitambulisho, wakati tayari vimeshazaliswa na NIDA, nashukuru.