Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 147 2024-02-09

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, lini mradi wa maji wa vijiji 19 maarufu kama Dambia utaisha?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tayari imeanza utekelezaji wa Mradi wa Maji, Dambia – Haydom unaolenga kunufaisha vijiji 19 vya Yaeda Kati, Dirim, Endalat, Endamily, Murkuchida, Endanachan, Basonyagwe, Basoderer, Bashay, Qandach, Ng'wandakw, Haydom, Garbabi, Yaeda Chini, Mongo wa Mono, Domanga, Eshkesh, Endagulda na Harar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa matenki matano yenye jumla ya lita 2,675,000; ulazaji wa bomba kuu la kupeleka maji kwenye tenki umbali wa kilometa 8.7; ulazaji wa mabomba ya usambazaji umbali wa kilometa 357.5; ujenzi wa nyumba 1 ya mitambo (pump house) na ufungaji wa umeme; ujenzi wa ofisi ya chombo cha watumiaji maji, ujenzi wa vituo 192 vya kutolea huduma ya maji vyenye mfumo wa malipo ya kabla (prepaid water meters); ujenzi wa mbauti nne za kunyweshea mifugo; pamoja na ufungaji wa pampu nne za kusukuma maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huo upo kwenye hatua za awali za utekelezaji ambapo unatarajiwa kukamilika Mwezi Oktoba, 2025 na kunufaisha wananchi wapatao 133,737. (Makofi)