Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini mradi wa maji wa vijiji 19 maarufu kama Dambia utaisha?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, lakini kwanza, nishukuru kwa hatua na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna vijiji vya Getesh, Qamtananat, Gidbiyo, Dotina, Qaloda, Geterer, Muslur, Endanyawish, Maretadu na Qatros. Je, lini unavipatia fedha ili kupata maji katika vijiji nilivyovitaja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa sasa vijiji nilivyotaja ni vingi na fedha umezitoa; je, ni lini sasa tunaambatana ili kufanya ziara katika maeneo haya uliyoyataja?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa ambayo ameifanya hasa juu ya kupigania mradi huu wa Dambia, lakini kubwa katika vijiji ambavyo amevieleza nataka nimuhakikishie utekelezaji wa Miradi ya Maji unategemeana na fedha. Tutatoa fedha juu ya ujenzi wa miradi hiyo hasa katika vijiji vyake ili wananchi wake waweze kupata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ameniomba kwenda, nipo tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge hasa katika Jimbo lake la Mbulu Vijijini kwenda kutazama ufuatiliaji wa ujenzi wa mradi huu wa maji.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini mradi wa maji wa vijiji 19 maarufu kama Dambia utaisha?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, niipongeze Serikali kwa ujenzi wa visima vya Kimbiji na Mpera. Mradi ule ni wa muda mrefu lakini umekamilika tunaipongeza sana Serikali. Mradi huo kukamilika kwake kumepelekea kupatikana kwa maji ya bomba safi na salama katika Kijiji cha Tungi Songani, Kata ya Pembamnazi, Wilaya ya Kigamboni, lakini kumekuwa na changamoto ya kutopatikana maji hayo sasa pamoja na kujengwa kwa mradi ule katika eneo hilo na wananchi walipata maji haya kwa muda na sasa hawapati tena.

Je, Serikali ina kauli gani kuhusiana na changamoto hiyo inayowakuta akina mama wa Pembamnazi Kijiji cha Tundu Songani, kukosa huduma hiyo ya maji safi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, Mama yangu Mariam. Ni kweli katika Eneo la Kigamboni tumejenga mradi mkubwa takribani wa tanki la lita milioni 15 kwa ajili ya kuhakikisha wana-Kigamboni wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata hii taarifa, kwa kuwa ni mpya naomba niipokee na niweze kuifanyia ufuatiliaji kwa haraka ili kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo ya Kigamboni wanaenda kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini mradi wa maji wa vijiji 19 maarufu kama Dambia utaisha?

Supplementary Question 3

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa uniona, sisi Jimbo la Buchosa tuna shukrani nyingi sana kwa Serikali kwa miradi mingi ya maji ambayo imejengwa, lakini tunasikitika kwamba, Mradi wa Bugoro, Nipandwa, Kafunzwe na Kazuzu ambayo thamani yake ni karibu bilioni 22 sasa imesimama na yako madai kwamba, wakandarasi hawajalipwa.

Je, watalipwa lini ili miradi hii iweze kukamilika kabla ya uchaguzi wa Serikali za mitaa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kwamba, tumeshapokea bilioni 27, hasa kwa ajili ya kuwalipa wakandarasi. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Kaka yangu Shigongo kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kule Buchosa, nitaenda kumuunga mkono hasa kulipa wakandarasi wake ili waweze kuendeleza kazi nzuri ambayo anaifanya katika Jimbo lake la Buchosa.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini mradi wa maji wa vijiji 19 maarufu kama Dambia utaisha?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, mimi kwanza naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwatua akina mama wa Mchinga ndoo kichwani. Sambamba na hilo nimshukuru Mheshimiwa Waziri wa Maji, ule mradi umekamilika kwa asilimia kubwa.

Je, ni lini Mheshimiwa Waziri utakuja kwenye Jimbo la Mchinga kwa ajili ya uzinduzi wa mradi ule?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jambo kubwa ambalo wana-Mchinga wanatakiwa kumkumbuka Mheshimiwa Mbunge wao ni juu ya suala la maji la mradi huo mkubwa. Nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge nipo tayari kuambatana na wewe hasa katika kwenda kukagua Mradi huo wa Mchinga. Ahsante sana.