Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 148 2024-02-09

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, lini Bwawa la Mwanjoro litakarabatiwa ili kuwezesha usambazaji wa maji Vijiji vya Jinamo na Witamihya - Meatu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vya Jinamo na Witamihya kwa sasa vinapata huduma ya maji kupitia kisima chenye uwezo wa kuzalisha maji wastani wa lita 24,000 kwa siku. Katika muendelezo wa kuboresha huduma ya maji katika vijiji hivyo Serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 itatenga fedha kwa ajili ya kukarabati Bwawa la Mwanjoro, ili kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa maji katika Vijiji vya Mwanjoro, Jinamo na Witamihya vyenye jumla ya wakazi 5,002. Kazi zinazotarajiwa kutekelezwa katika ukarabati wa bwawa hilo ni pamoja na ukarabati wa tuta umbali wa mita 100 (embankment), ukarabati wa utoro wa maji (spill way) na uimarishaji wa kingo za tuta la bwawa (side slopes).