Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, lini Bwawa la Mwanjoro litakarabatiwa ili kuwezesha usambazaji wa maji Vijiji vya Jinamo na Witamihya - Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninashukuru majibu ya Serikali. Ninamshukuru Mheshimiwa Rais kwa kutupatia shilingi bilioni moja na milioni 500 kwa ajili ya kunusuru Mji wa Mwanuzi, lakini pia ametuongezea milioni 500 kwa ajili ya kuongeza kina cha maji katika Mji wa Mwanuzi na Kijiji cha Lukale, ambacho sasa wanapata maji safi. Ninayo maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali gharama ya ukarabati huu wa Mradi huu wa Mwanjoro ni kubwa sana.

Je, Serikali iko tayari kutenga bajeti yake katika Serikali Kuu, ili kutokuathiri bajeti ya RUWASA?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Nimshukuru sana Mheshimiwa Aweso kwa kazi nzuri na wepesi wake. Mji wa Mwanuzi tayari tuna maji ya kutosha ya bwawa na kisima, treatment plant ni nzuri, pumps zote ni nzuri. Nilitaka kumuomba Mheshimiwa Waziri, Je, yuko tayari kufika Mji wa Mwanuzi na kuona kwa nini kuna mgawo mkubwa wa maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kwa kweli kumpongeza Mheshimiwa Mbunge wa Meatu. Tumefanya ziara maeneo mengi sana, lakini nilivyofika Meatu nimeshuhudia wapo watu wanapata shida ya maji lakini Meatu walikuwa na dhiki ya maji; Lakini kupitia Mheshimiwa Mbunge Leah Komanya kwa kazi aliyoifanya kwa kweli, Mama Leah Komanya Mungu akupe maua yako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kikubwa katika suala hili la kuchukua bajeti juu ya ujenzi wa Bwawa la Mwanjoro, nataka nimhakikishie sisi Wizara ya maji tupo tayari kuibeba bajeti hiyo juu ya ujenzi wa bwawa hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini juu ya kwenda na mimi katika Eneo lake la Meatu nipo tayari na ninataka niwatake watendaji wa Meatu, kazi ambayo imefanyika juu ya kutatua tatizo la maji Meatu ni kubwa. Kuona sasahivi kuna mgawo wa maji haikubaliki hata kidogo kwa hiyo, wajitathmini na sisi tupo tayari kwenda na kama kuna uzembe wowote tutachukua hatua ya haraka, ili kuhakikisha kwamba wananchi wa Meatu wanaendelea kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, lini Bwawa la Mwanjoro litakarabatiwa ili kuwezesha usambazaji wa maji Vijiji vya Jinamo na Witamihya - Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ziada kwanza niseme pongezi sana kwa Mheshimiwa Rais kwa kunijengea matanki mawili Mshikamano na Tegeta A kwa kuwasaidia wananchi lakini sasa bado kilio cha miaka miwili kuhusu usambazaji wa mabomba kwa wananchi, mahitaji ni bilioni tano, uwezo wa ndani bilioni mbili tayari.

Je, Wizara mko tayari kutoa kauli kuisaidia DAWASA bilioni tatu, ili wakamilishe usambazaji wa mabomba kwa wananchi wale?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa kweli kazi ambayo ameifanya Kibamba Mheshimiwa Mbunge ni kubwa na DAWASA kazi wanayoifanya katika jimbo lake ni kubwa, kazi iliyobaki ni usambazaji. Sisi kama Wizara ya maji tupo tayari kushirikiana na DAWASA katika kuhakikisha tunamaliza tatizo la maji hasa katika eneo la Kibamba. Ahsante sana.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, lini Bwawa la Mwanjoro litakarabatiwa ili kuwezesha usambazaji wa maji Vijiji vya Jinamo na Witamihya - Meatu?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na kazi nzuri inayofanywa katika Mradi wa Makonde, katika bajeti ya mwa 2022/2023 Wizara ilipanga kujenga mabwawa kumi kwa kutumia force account nchini.

Je, ni lini ujenzi wa Bwawa la Lukuledi – Masasi ambalo lilipitishwa katika Bunge lako Tukufu ujenzi huo utaanza?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kwa mara nyingine kumshukuru Mheshimiwa Agnes Hokororo, kwa kweli amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana juu ya changamoto ya maji, hasa maeneo ya Mtwara, lakini juu ya ujenzi pia wa bwawa hili la Lukuledi. Nataka nimhakikishie, Wizara ya maji hatuna kisingizio, tumepata mitambo ya uchimbaji visima na mitambo ya ujenzi wa mabwawa. Nataka nimhakikishie hii kazi tutaianza kwa haraka, ili Bwawa hili la Lukuledi tunalianza na wananchi hawa waende kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, lini Bwawa la Mwanjoro litakarabatiwa ili kuwezesha usambazaji wa maji Vijiji vya Jinamo na Witamihya - Meatu?

Supplementary Question 4

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Bwawa la Maji la Ichemba, tunashukuru Mungu limepewa bajeti ya kujengwa lakini tatizo mkataba ulioingiwa wa kujenga lile bwawa ulikuwa na kodi ya ongezeko la thamani.

Je, ni lini sasa hili ongezeko la thamani or VAT inclusive litaondolewa, ili huyu mkandarasi aweze kuanza kazi kwa wakati? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa ambayo ameifanya, nimuombe sasa labda tukutane ofisini, ili tuweze kulishughulikia hili jambo kwa haraka ili ujenzi wa bwawa hili uanze mara moja na wananchi wake waende kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, lini Bwawa la Mwanjoro litakarabatiwa ili kuwezesha usambazaji wa maji Vijiji vya Jinamo na Witamihya - Meatu?

Supplementary Question 5

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Wananchi wa Kijiji cha Wosiwosi, Wilayani Longido hususan akina mama wana changamoto kubwa ya kupata maji safi na salama.

Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi yake ya kuwachimbia bwawa wananchi hawa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru na niendelee kumpongeza Mheshimiwa Zaytun Swai na ninataka nimhakikishie kwamba kesho tutakuwa Longido, tutatoa commitment yetu; na swali hilo ambalo ameelekeza na sisi kama mitambo tuliyokuwanayo tutajitahidi kuhakikisha kwamba inakwenda na wananchi hawa wachimbiwe bwawa na wananchi waende kupata huduma ya maji safi na salama.