Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 149 2024-02-09

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: -

Je, lini Serikali itafunga laini ya pili ya umeme kutoka Geita hadi Sengerema ili kutatua tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tabasam Hamis Mwagao, Mbunge wa Sengerema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo awali Wilaya ya Sengerema ilikuwa ikipata umeme kutokea Mwanza Mjini kupitia njia ya umeme iliyokuwa inapita chini ya Ziwa Victoria. Aidha, wakati wa ujenzi wa Daraja la Kigongo Busisi, kwa bahati mbaya mkandarasi alikata submarine cable na tangu wakati huo Sengerema ikawa inapata umeme kutoka kituo kipya cha kupoza umeme cha Geita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO imekubaliana na Mkandarasi kuweka sehemu ya kupitisha waya pembeni mwa Daraja la Kigongo – Busisi ambapo waya huo utapitishwa badala ya kupita kwenye maji. Aidha, kazi hiyo itafanyika baada ya kukamilika kwa ujenzi wa daraja na kuwezesha Wilaya ya Sengerema kuendelea kupata umeme kutokea Mwanza Mjini kama ilivyokuwa awali.